Timu ya wanamichezo takribani 126 kutoka Mkoani Geita, inatarajiwa kuanza safari ya kuelekea Mkoani Iringa ambapo itashiriki mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania UMITASHUMTA kwa ngazi ya Kitaifa, yatakayoanza kutimua vumbi mnamo tarehe 7, Mwezi Juni.
Akizungumza wakati akifunga mashindano hayo kwa ngazi ya Kimkoa mapema wiki hii katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu, Katibu Tawala Mkoa, Bw. Mohamed Gombati ameipongeza Halmashauri ya Wilaya Ya Geita, pamoja na kutoa rai kwa Halmashauri zote kuweka mipango endelevu ya kukuza na kuendeleza michezo mashuleni.
Mashindano hayo yatahusisha Mchezo wa Soka, Mpira wa Pete, Mpira wa Kikapu, Mpira wa Mikono, Mpira wa Wavu, Riadha na Fani za Ndani.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa