• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YA UVIKO 19 GEITA DC YAWAKOSHA WAJUMBE WA KAMATI YA SIASA MKOA WA GEITA

Posted on: January 14th, 2022

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita Januari 14, 2022 imefanya ziara ya kukagua Miradi iliyojengwa kwa fedha za UVIKO 19 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita na kueleza kuridhishwa na ubora wa Miradi hiyo.

Kiongozi wa msafara wa ziara hiyo ambaye ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa kutoka Mkoa wa Geita Bw.Evarist Gervas ameeleza wazi kuridhishwa na thamani na ubora wa Miradi hiyo huku akiisifu Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kusimamia vizuri ujenzi wa Miradi hiyo.

Bw.Evarist amesema kuwa Viongozi wana wajibu wa kutangaza mazuri yaliyofanywa na Serikali ili jamii itambue namna Rais Samia anavyowajali wananchi wake kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ya jamii kama alivyofanya kupitia Fedha za UVIKO 19.

Aidha ametoa wito kwa Wazazi kuhakikisha wanadhibiti utoro kwa kuwapeleka watoto wao shuleni sambamba na kuwataka walimu kufundisha kwa bidii ili madarasa hayo yaliyojengwa kwa gharama kubwa na ubora wa hali ya juu yalete matokeo mazuri.

Bw.Evarist akiwa katika kata ya Rwamgasa alipotembelea Mradi wa vyumba 14 vya madarasa katika shule ya sekondari Isingiro ameunga mkono juhudi za wananchi katika kuchangia Maendeleo kwa kutoa  kiasi cha shilingi laki tano ambapo awali alitoa wito wa kusimamia vizuri Miradi ya maendeleo inayojengwa kwa nguvu za wananchi ili iwe na ubora kama Miradi inayoletewa fedha na Serikali Kuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe.Wilson Shimo akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita ameendelea kutoa shukrani kwa Rais Samia kwa fedha nyingi alizoupatia Mkoa wa Geita huku akiwataka wananchi kutembea vifua mbele kwa kuwa hakuna vikwazo kwa watoto wetu kuanza kidato cha kwanza.

‘‘Shime wazazi tuwapeleke na kuwahimiza watoto wetu kuja shuleni kusoma shule zitakapofunguliwa na mwisho tutegemee ufaulu kwani kwa miundo mbinu hii mizuri, ni wazi mwanafunzi atakayeanzia kusomea humu sidhani kama atafeli ”.

Naye mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Geita Bw.Lucas Mazinzi amechangia mifuko 10 ya Saruji katika shule hiyo ya sekondari Isingiro huku akiisifu Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kazi kubwa ya usimamizi wa ujenzi wa Miradi hiyo iliyofanywa usiku na mchana huku akiomba kupewa mbinu ya ufanisi kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilikuwa na Miradi mingi zaidi ingawa imekamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita John Paul Wanga akiwa katika ziara hiyo amemshukuru Rais Samia kwa kuipatia Halmashauri hiyo kiasi cha shilingi Bilioni 7 na Milioni 120 kwa kipindi cha Julai hadi Disemba 2021 iliyowezesha kujenga Miradi mbalimbali ya maendeleo.

Fedha hizo zimesadia kukamilisha ujenzi wa vyumba 347 vya madarasa kwa shule 44 za sekondari na vyumba 5 vya madarasa  kwa ajili ya shule mbili shikizi za msingi na bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule ya sekondari Katoro.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe.Charles Kazungu akizungumza wakati wa kuhitimisha ziara hiyo ameshukuru kwa pongezi zilizotolewa kwa Halmashauri hiyo huku akiahidi kutobweteka na badala yake wataendelea kutekeleza kikamilifu Ilani ya Chama Cha Mapinduzi sambamba na kupokea ushauri wanaopewa na viongozi mbalimbali.

Kamati hiyo ya Siasa Mkoa wa Geita ilitembelea na kukagua Miradi ya ujenzi wa kituo cha Afya Bugalama wenye thamani ya shilingi milioni 250, Mradi wa vyumba 13 vya madarasa katika shule ya sekondari Bugalama wenye thamani ya shilingi milioni 260, na Mradi wa vyumba 8 vya madarasa katika shule ya sekondari Chigunga wenye thamani ya shilingi milioni 160.

Aidha kamati hiyo iliendelea kukagua Mradi wa vyumba 6 vya madarasa katika shule ya sekondari Butundwe wenye thamani ya shilingi milioni 120, na kuhitimisha na Mradi wa vyumba 14 vya madarasa katika shule ya sekondari Isingiro wenye thamani ya shilingi milioni 280 amabapo kamati hiyo imeridhishwa na miradi yote hiyo.



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa