• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YA MAENDELEO GEITA DC YAMRIDHISHA MNEC NADRA RASHIDI

Posted on: September 30th, 2023

Na Hendrick Msangi

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi (CCM) na mwakilishi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Nadra Gulam Rashid, amefanya ziara Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Katika Ziara hiyo ya kukagua miradi inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita, MNEC Nadra aliambatana na viongozi wengine wa chama na serikali

Ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo chini ya Serikali yao inayoongozwa na Mheshiwa Dkt Samia  Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MNEC huyo alipokea taarifa ya Ujenzi  wa Miundombinu ya Afya Katika Hospitali ya Nzera,  Ujenzi  wa Hospitali hii umefanyika kupitia awamu tatu tofauti kulingana na Mapokezi ya fedha kutoka Serikali Kuu  ambapo Jumla ya Tzs 2,806,000,000 zilipokelewa kutoka OR TAMISEMI kupitia fedha za bajeti ya Serikali  mpango wa UVIKO 19 na SRWSS, ilisema taarifa hiyo ya  Dkt Modest Buchard (MD.MPH) ambaye ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Geita

Aidha katika taarifa hiyo ya Utekelezaji wa Mradi huo, Dk Buchard alimueleza Mwenyekiti UWT , Ujenzi huo ambao umefanyika katika awamu tatu, umegharimu kiasi cha shilingi 1,500,000,000 kwa majengo saba ambayo ni Jengo La Utawala, Jengo la Wagonjwa wa Nje, Jengo la Maabara, Jengo la Ufuaji, Jengo la Mionzi, Wodi ya Wazazi na Jengo la Kuhifadhia dawa ambapo yote yamekamilika.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Modest Buchard akimtembeza MNEC Nadra Rashidi kukagua miradi ya maendeleo Hospitali ya Nzera.

Akiendelea katika taarifa hiyo, Dkt Buchard alisema  awamu ya pili ilihusisha ujenzi wa  wodi tatu za wanawake , wanaume na wodi ya watoto, ambapo Serikali kuu iliipatia  Halmashauri  kiasi cha shilingi 500,000,000 huku akitaja kutokamilika kwa ujenzi huo kutokana na kupungua kwa fedha zilizopokelewa.

Dkt Buchard alimueleza MNEC huyo, kuwa Halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi 250,000,000 kupitia mpango wa UVIKO 19 kwa ajili ya awamu ya tatu ya ujenzi wa Jengo la wagonjwa mahututi(ICU) ambapo jengo hilo limeshakamilika  na kuanza kutumika. Ujenzi mwingine uliokamilika katika awamu hiyo ni Ujenzi wa Kichomea taka cha kisasa (High Tech Incinerators), shimo la kutupia kondo la nyuma na shimo la majivu ambapo gharama za ujenzi zilikuwa jumla ya shilingi 56,000,000 ambazo zilipatikana kupitia progamu ya SRWSS.

Kupitia serikali Kuu inayoongozwa na Mh Dkt Samia  Suluhu Hassan, hospitali hiyo imepokea  vifaa tiba vya kisasa kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa wanachi vikiwemo vifaa vya upasuaji, vifaa vya kujifungulia, vifaa kwa ajili ya wagonjwa mahututi  pamoja na huduma ya vifaa vya mionzi (X Rays)

Akipokea taarifa hiyo, MNEC Nadra Gulam Rashid, alisema, Serikali inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imejipanga kuwafikia wananchi wote katika ngazi zote kuhakikisha huduma bora za afya, elimu , maji, miundombinu ya barabara na nishati ya umeme vinapatikana


MNEC Nadra Rashidi akipitia taarifa ya miradi iliyotekelezwa na Halmashauri ya Wilya ya Geita

Katika ziara hiyo ambayo baadaye ilifuatiwa na mkutano wa hadhara katika kata ya Nzera, Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Mh Joseph Musukuma, alimshukuru MNEC huyo ambaye alikuwa akimuwakilisha Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) mama Mary Chatanda aliyekuwa kwenye kata nyingine za Halmashauri hiyo huku akimtaka amfikishie salaam za shukrani Mh Dkt Samia  kwa kuwaletea maendeleo wana Geita-DC  ambapo idadi ya Shule za Sekondari imeongezeka, uboreshaji wa huduma za afya na miundombinu ambapo wakandarasi wapo site kuendelea na kazi.

Aidha Mh Musukuma aliwasihi wananchi hao wa kata ya Nzera kuipa serikali yao muda na kuwahikikishia kupata huduma bora za kijamii likiwepo tatizo la umeme ambalo limekuwa ni kero kubwa.

Katika ziara hiyo iliyofanyika kwenye kata mbali mbali za Halmashauri ya Wilaya ya Geita, MNEC huyo pamoja na ujumbe wake waliweza pokea taarifa mbalimbali kutoka kwa wahusika waliopewa dhamana ya kusimamia miradi hiyo katika maeneo tofauti ya Halmashauri ya Geita DC.

Miradi mingine iliyotolewa taarifa kwa wajumbe hao waliofika kata tofauti za Halmashauri ya Geita DC ni pamoja na Ujenzi wa Miundombinu ya Kidato cha tano na sita shule ya Sekondari Butundwe yenye jumla ya wanafunzi 910 na walimu 22 ambapo ujenzi wake umefadhiliwa na Kampuni ya Barrick-Tanzania kwa gharama ya shilingi 487,300,000. Mradi huo haujakamilika kutokana na changamoto ya ucheleweshwaji wa malipo kwa mkandarasi.

Mradi wa ujenzi wa Bweni la Wasichana shule ya Sekondari Nyakagwe yenye jumla ya wanafunzi 175 ambao ujenzi wake umegharimu kiasi cha shilingi 157,084,142.85 huku kiasi cha shilingi 17,550,000.00 sawa na asilimia 10 % ilichangiwa na wananchi na kiasi cha shilingi 139,534,142.85 sawa na asilimia 90% ilitolewa na mfuko wa maendeleo (TASAF). Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100% ingawa bweni hilo halijaanza kutumika kutokana na changamoto za huduma ya umeme na maji.

MNEC Nadra alihitimisha ziara yake kwa kutembelea mradi wa kituo cha afya cha Kakubilo  unaokadiriwa kuwa na gharama zinazofika kiasi cha shilingi 115,143,505  gharama hizo zikiwa ni nguvu ya wananchi, Halmashauri na CSR kupitia mgodi wa dhahabu Geita Gold Mine Limited (GGML).

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa