Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya Taifa, Mhe. Steven Wasira, amesema kuwa, mojawapo ya ajenda kuu ya Serikali ya Awamu ya Sita ni pamoja na kuhakikisha inasimamia vyema maendeleo ya wananchi ili kusudi iweze kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.
Akizungumza Juni 17 katika mwendelezo wa ziara yake ya Kanda ya Ziwa eneo la Mji Mdogo Katoro, Mhe. Wasira amesema kuwa, CCM ikiwa kama chama kilichobeba matumaini ya Watanzania, kina wajibu wa kusikiliza wananchi, na kuwaletea maendeleo kwa vitendo kwa kuwa ndicho chama kilichopo madarakani.
Mhe. Wasira pia ameongeza kwa kusema kuwa, tangu Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Raisi Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan iingie madarakani, imeweza kukamilisha Miradi mikubwa ikiwemo Reli ya Mwendokasi (SGR), Bwawa la Kufulia Umeme la Mwalimu Nyerere (JNHPP), pamoja na Daraja la Busisi ambalo linatarajiwa kuanza kutumika hivi karibuni.
Aidha, ameongeza kwa kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kusimamia ujenzi wa Shule mpya za Msingi Saba (7), pamoja na za ngazi ya Sekondari Tisa (9) eneo la Katoro, huku pia Serikali ikiwa mbioni kuboresha huduma za Maji kwa kuunganisha mabomba kutoka kijiji cha Chankorongo, kuja Katoro.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa