• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MHE MSUKUMA AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI IBADA YA MAZISHI YA ALIYEKUWA DIWANI WA KATA YA NYAMBOGE

Posted on: July 3rd, 2024

MBUNGE wa Jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Msukuma Julai 3, 2024, ameungana na waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Watumishi wa Halmashauri, Viongozi wa Chama na Serikali,ndugu jamaa na marafiki katika ibada ya Misa takatifu ya kuaga mwili wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Nyamboge Mhe Daud Simon Mlekwa aliyefariki June 30,2024 katika hospital ya Wilaya ya Geita -Nzera alipokuwa akipatiwa matibabu.

 

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Kasheku Msukuma as amewaasa wanananchi wa Kata ya Nyamboge kutojihusisha na tabia za kuwakata mapanga watu wenye Ulemavu na kuwataka kuwafichua wale wote wanaojihusisha na tabia hizo. Msukuma pia ameeleza kusikitishwa kwake na msiba wa Diwani Daud Mlekwa na kuwaahidi Wananchi kuendeleza Miradi yote ambayo marehemu Mlekwa alikuwa akiisimamia katika kata hiyo.

Marehemu Mlekwa amekuwa Diwani wa Kata ya Nyamboge kwa kipindi cha miaka 9 toka mwaka 2015 kupitia chama Cha Mapinduzi (CCM)  hadi umauti ulipomkuta  akiwa bado ni Diwani wa Kata hiyo.


Wakizingumza kwa nyakati tofauti Viongozi wa Chama na Serikali wamemuelezea  Diwani Mlekwa kuwa Kiongozi aliyewaunganisha Wananchi wa Kata ya Nyamboge kwa kushirikiana na wananchi na Halmashauri katika Kutekeleza Miradi ya Maendeleo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Salige Mkome amewaeleza mamia ya waombolezaji  kuwa Halmashauri imepoteza Kiongozi aliyekuwa jemedari ,mwadilifu na mchapa kazi aliyeshirikiana na uongozi wa Halmashauri katika utekelezaji wa Shughuli za Maendeleo katika kata ya Nyamboge.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Salige Mkome amesema Marehemu Daud Mlekwa alikuwa Kiongozi jemedari mwadilifu na mchapa kazi katika kusimamia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo katika kata ya Nyamboge na kuongeza kuwa atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Naye Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita Cde Gabriel Nyasilu amesema kama chama kimepata maumivu kwa kumpoteza Kiongozi aliyewaunganisha wananchi na kutoa pole kwa Madiwani na uongozi wa Halmashauri kwa msiba huo mzito.

Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita Komredi Gabriel Nyasilu amesema chama Cha Mapinduzi kimepata maumivu kwa kumpoteza Kiongozi aliyewaunganisha wananchi Katika kuleta Maendeleo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Hadija Said amesema marehemu Daud Mlekwa alikuwa kiungo kikubwa katika baraza la Madiwani katika utendaji kazi wake na kuwataka Wananchi wa Kata hiyo kuendelea kuyaenzi  aliyokuwa akiyafanya na kuwahakikishia Miradi ya Maendeleo itaendelea Kutekelezwa  na kuwataka wananchi kuwa watulivu.

 Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Hadija Said amesema marehemu Daud Mlekwa alikuwa kiungo kikubwa katika baraza la Madiwani na kuwataka wananchi wa kata ya Nyamboge kuendeleza mazuri yote aliyoyaacha Marehemu Mlekwa.

Akizungumza katika Ibada ya Mazishi iliyofanyika Nyumbani kwa marehemu Mlekwa kijiji cha Chalameno kata ya Nyamboge Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Kasheku Musukuma ametoa pole kwa Madiwani kwa kipindi kigumu walichopitia kwa kupoteza Madiwani wawili kwa kipindi kifupu ikiwepo kifo cha aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kamena Marehemu Peter Kulwa aliyefariki June 13, 2024.


Aidha amesema Serikali na chama vitaendelea Kutekeleza Miradi ya Maendeleo na kuwaahidi Wananchi wa Kata hiyo kuendelea kusimamia yale yote ambayo marehemu Mlekwa aliwaahidi wananchi wa Nyamboge.


Pia Mhe Msukuma ametumia nafasi hiyo kuwaasa Wananchi kuacha tabia za kukata mapanga watu wenye Ulemavu wa ngozi na kuwataka wananchi kuwafichua wale wote wenye tabia za kuwakata watu mapanga.


Marehemu Mlekwa ataendelea kukumbukwa kwa mchango wake mkubwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika kusimamia utekelezaji wa Shughuli za Maendeleo ndani ya Halmashauri.

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa katika hali ya huzuni na simanzi Katika Misa takatifu ya kuaga mwili wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Nyamboge Mhe Daud Mlekwa aliyefariki June 30,2024 katika hospital ya Wilaya ya Geita -Nzera alipokuwa akipatiwa matibabu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa