• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MCHENGERWA ATOA MAAGIZO KWA WAKURUGENZI GEITA

Posted on: December 21st, 2023

Na Hendrick Msangi

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (MB), Desemba 16, 2023 amefanya ziara ya kikazi Mkoani Geita ambapo katika ziara hiyo amefanya kikao na viongozi wa Mkoa pamoja na kuzungumza na Watumishi wa sekretarieti ya Mkoa.


Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia hotuba ya Waziri Mchengerwa.

Katika kikao hicho ambacho Halmashauri zote za Mkoa wa Geita zilishiriki zikiongozwa na wenye viti wa Halmashauri,Wakurugenzi watendaji, pamoja Wakuu wa Wilaya, ziliweza  kukabidhiwa magari matano ya usimamizi wa shughuli za Afya pamoja na vifaa vya TEHAMA kwa vituo vya walimu kwenye Halmashauri zote za mkoa wa Geita.

Mhe Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mohamed Omary Mchengerwa (MB) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Cornel Magembe funguo za gari kwa ajili ya usimamizi Shirikishi kwa Shughuli za Afya.

Waziri huyo alitumia nafasi hiyo kuwataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii katika maeneo yao, ili kumtendea haki Mhe Rais kwa kuwasikiliza wananchi kero zao, kuwa na nidhamu kazini, kujishusha, kuwa wanyenyekevu , kuwa na huruma,  kujiepusha na vitendo vya rushwa ambavyo hupelekea mambo mengi kuharibika na kusababisha serikali kuchukiwa. “Atakaye fanya kazi kwa bidii tutamlinda kwa nguvu zetu zote kwa kumsaidia kwa kuwa anafanya kazi vizuri na kwa bidii” alisema Mhe Mchengerwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro akipokea Kompyuta kutoka kwa Waziri wa nchi OR-TAMISEMI Mhe Mohamed Omary Mchengerwa kwa ajili ya Vituo vya Walimu kwenye Halmashauri za Mkoa wa Geita.

Akiendelea katika hotuba yake kwa watumishi hao, Mhe Mchengerwa (MB), aliwaagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa huo kuwa na mpango wa kuandaa vyanzo vipya viwili vya mapato ambavyo kila Mkurugenzi atapimwa kwa namna ambavyo ataweza kubuni vyanzo vipya vya mapato.”Wakurugenzi muende mkajipange kila mwaka tutakuwa tuna angalia umekuja na vyanzo vipya vya mapato na iwapo vitakuwa havijatimia itapelekea kuwekwa pembeni ama kutafutiwa kazi nyingine itakayakutosheleza kutokana na uwezo wako”, alisema Mhe Waziri.

Kuhusu swala la Miradi ambayo serikali inatenga fedha nyingi, Mhe Mchengerwa alisema zitaandaliwa fomu maalumu ambazo Mkurugenzi, Mhandisi na mtu wa Manunuzi watazisaini kama uthibitisho wa kukubali fedha hizo kutosheleza kutekeleza miradi iliyopangwa ili kuepuka upotevu wa fedha ambao umekuwa ukijitokeza maeneo mengine na kusababisha kutokamilika kwa miradi.

Aidha aliwataka Wakurugenzi Katika mpango wa maendeleo kutenga bajeti kwa ajili ya watumishi wanaoenda likizo kwa kuwaandalia stahiki zao na sio kuwakopesha kuepusha makasiriko kwa watumishi na kuepelekea watumishi kuichukia serikali yao. 

Pia alielekeza fedha zinazokusanywa kutenga asilimia zitakozokwenda kwenye mipango ya maendeleo katika Halmashauri zao na sio kusubiri bajeti ya serikali.

Pamoja na kukabidhi magari hayo, Mhe Mchengerwa (MB), ametoa wiki mbili kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambao hawaishi kwenye maeneo yao ya kazi kunakopelekea wananchi kukosa huduma kwa wakati kurejea kwenye maeneo yao na iwapo watashindwa kufanya hivyo watahamishwa kupelekwa maeneo mengine, huku akimuagiza Mkuu wa Mkoa Ndugu Martine Shigela kuandaa taarifa ya watumishi ambao hawakai maeneo yao ya kazi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Musukuma ambaye aliwawakilisha wabunge wa mkoa huo, aliipongeza serikali ya awamu ya sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo alisema amefarijika sana kushirki kikao hicho ambacho Mhe Waziri alikabidhi magari kwa Halmashauri za Mkoa huo nakuishukuru Serikali kwa niaba ya watumishi wa Mkoa huo, “ Hakuna Jimbo linalomdai Mhe Rais kwani tuna miradi mingi, Mhe Rais ametoa pesa kujenga Uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Mwanza pamoja na daraja ambapo kukamilika kwake  kutawezesha watalii kufika kwenye vivutio vya utalii vilivyopo Mkoani Geita kwa urahisi,” alisema Musukuma

Mkuu wa Mkoa Ndugu Martine Shigela aliishukuru serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuchangia huduma za elimu bila malipo katika Mkoa wa Geita, ukamilishaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo SEQUIP, BOOST, UVIKO na nyingine kutoka serikali kuu amabapo Mkoa wa Geita umepokea fedha nyingi zaidi ya Bilioni 47 ambazo zimewezesha kujenga shule mpya Zaidi ya 18 kwani ndio msingi wa maendeleo kwenye Taifa letu, Kwa upande wa Afya, Shigela alisema Mkoa wa Geita una Baraka kwani kuna Hospitali mbili za Wilaya moja ikiwa Nzera na nyingine Katoro zote zikiwa kwenye jimbo la Mhe Musukuma(MB) huku akitaja hospitali nyingine katika Halmashauri za Mbogwe, Nyang’wale, Bukombe ambapo zote serikali imetenga fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa.

Mkuu wa Mkoa wa Geita ndg Martine Shigela akiongea na Watumishi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Geita wakati wa Ziara ya Kikazi ya Mhe Waziri wa nchi OR-TAMISEMI alipotembelea Mkoa wa Geita.

Kuhusu swala la Lishe Mhe Mkuu wa mkoa alimueleza Mhe Waziri kuwa Mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa mitano ambayo haikufanya vizuri kwenye swala la lishe , ambapo hatua madhubuti zimeshachukuliwa  kwa kuweka mikakati pamoja na kuwa na nyenzo zote zinazohitajika kwenye vituo vya afya ikiwa ni pamoja na kuongeza hamasa.

Aidha alimuahidi Mhe Waziri kuyatunza Magari ambayo Serikali imetoa kwa Mkoa wa Geita zikiwepo Ambulance mbili ambazo tayari zimeshaanza kutoa huduma kwenye Halmashauri ya Mbogwe na Nyang’wale na mengine ambayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (MB) aliyakabidhi.

Naye msimamizi Mkuu wa shughuli za afya, Lishe na Ustawii katika Jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Modest Buchard, alitoa shukrani kwa awamu ya sita kwa kutoa magari matano ya usimamizi shirikishi kwa shughuli za afya na kumuahidi Mhe waziri kwenda kufanya kazi, kutumika ili kuendelea kumuunga mkono Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwani sio jambo ambalo limezoeleka.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa