• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MCHAKATO WA KUGAWA JIMBO LA BUSANDA SIO WA KISIASA BALI MAENDELEO-JAJI ASINA OMARI

Posted on: April 24th, 2025

Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi(INEC) , katika kutekeleza majukumu yake ya kisheria , imefanya kikao na wadau wa uchaguzi kutoka Halmshauri ya Wilaya ya Geita , kwa lengo la kujidhirisha kuhusu mchakato wa kugawa jimbo la Busanda kama ulifuata taratibu na vikao vya sheria.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Geita , Jaji wa Mahakama Kuu Mhe Asina Omari , kwa niaba ya mwenyekiti wa INEC , alisema kuwa tume ilipokea tume ilipokea rasmi maombi ya kugawa jimbo la Busanda kutoka kwa katibu tawala wa mkoa wa geita mnamo tarehe 28 februari 2025.

Jaji wa Mahakama Kuu Mhe Asina Omari  na mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi akizungumza katika Kikao  cha Mchakato wa Kugawa Jimbo la Busanda kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita

Kwa mujibu wa kanuni ya 18 ya kanuni za Tume ya mwaka 2024 , Jaji Asina alibainisha kuwa tume imeamua kutembelea baadhi ya majimbo yaliyoomba kugawanywa ili kuhakikisha kuwa  taarifa zilizowasilishwa ni sahihi na zinazingatia taratibu husika.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye pia Ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba (Kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Magaro wakati wa kikao cha Mchakato wa Ugawaji wa Jimbo la Busanda kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita

Katika kikao hicho , Adam Mkina , mwakilishi wa Mkurugenzi wa INEC , alitoa ufafanuzi kuhusu majina ya majimbo ,kata zinazohusika pamoja na ramani ya eneo linalopendekezwa kugawanywa. Wajumbe wa kikao hicho walithibitisha kuwa taarifa zilizowasilishwa na uongozi wa INEC zinaendana na maamuzi ya vikao vilivyopita na ni sahihi.

Bw. Adam Mkina , Mwakilishi wa Mkurugenzi wa INEC , alitoa ufafanuzi kuhusu majina ya majimbo katika Kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

Mchakato huu wa kugawanywa kwa jimbo la Busanda  umelenga kuboresha uwakilishi wa wananchi bungeni pamoja na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za kijamii. Jimbo la Busanda, ambalo limekuwa na ukubwa wa eneo na idadi kubwa ya wakazi, limekuwa likipokea maombi kutoka kwa viongozi na wananchi kuhusu kuligawa ili kuongeza uwakilishi na kuharakisha maendeleo.

Aidha , Wajumbe pia walitoa wito kwa serikali na mamlaka husika kuchukua jukumu la kuhakikisha kuwa mchakato huu unasimamiwa kikamilifu kwa uwazi na kwa kufuata taratibu zote, hadi pale majibu ya mwisho yatakapotolewa kuhusu hatma ya kuligawa Jimbo la Busanda. Wamesisitiza kuwa ni muhimu kila hatua ya mchakato huu ifanyike kwa kuzingatia usawa, maoni ya wananchi, na madhara chanya kwa maendeleo ya maeneo yote yanayohusika. Aidha, waliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa mrejesho kwa umma mara baada ya uchambuzi wa maoni kukamilika, ili wananchi wafahamu uamuzi wa mwisho na sababu zilizozingatiwa.

Pichani ni Wajumbe mbalimbali wakifuatalia Mchakato wa Ugawaji wa Jimbo la Busanda 

Jaji Asina Omari, akitoa neno la mwisho katika mkutano huo, alisisitiza umuhimu wa kufuata misingi ya haki, usawa na ushirikishwaji katika mchakato mzima wa kuligawa Jimbo la Busanda. Alieleza kuwa, "Mchakato huu si wa kisiasa bali ni wa kimaendeleo, na ni lazima usimamiwe kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi ananufaika na uamuzi utakaofanyika. Tume yetu itazingatia kila hoja, kila maoni, na kila ushahidi uliowasilishwa kabla ya kutoa mapendekezo ya mwisho."

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MHE. WASIRA: AJENDA YA SERIKALI NI KUSIMAMIA MAENDELEO YA WANANCHI.

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YAPATA HATI SAFI, MHE. FATMA APONGEZA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA.

    June 13, 2025
  • UFUATILIAJI WAHIMIZWA KWENYE USIMAMIZI WA MIRADI WILAYA YA GEITA

    June 12, 2025
  • MKURUGENZI ASISITIZA HATUA KUCHUKULIWA KUDHIBITI UTORO SHULENI.

    June 05, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa