• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAPATO YA NDANI YAWEZESHA UPATIKANAJI WA PIKIPIKI 23 ZENYE THAMANI ZAIDI YA MILIONI SABINI NA MBILI –GEITA DC

Posted on: January 5th, 2024

Na Hendrick Msangi

WATENDAJI wa Kata Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Januari 05, 2024 wamekabidhiwa pikipiki kwa ajili ya kuwawezesha katika shughuli zao za kila siku katika halmashauri ya wilaya ya Geita.

Akikabidhi pikipiki hizo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe Zephania Milimo Masele ambaye ni diwani wa kata ya Nzera yalipo makao makuu ya Halmashauri amewataka watendaji hao kufanya kazi kwa bidii kwa kuwatumikia wananchi.

Zephania Milimo Masele Diwani wa kata ya Nzera wa kwanza kushoto akisoma nyaraka wakati wa kukabidhi pikipiki 23 zilizotolewa kwa Watendaji wa kata

“Mkafanye kazi kwa bidii mkawahudumie wananchi na sio kuzitumia pikipiki mlizopewa katika biashara ya bodaboda, pia mzitunze na kuwa waangalifu mnapozitumia, pikipiki hizi zikawasaidie kufanya majukumu yenu ya kila siku na muweze kufika kwenye matukio kwa wakati kutekeleza majukumu yenu” alisema Masele

Aidha Diwani huyo alitumia nafasi hiyo kumshukuru Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha mazingira mazuri kwa watumishi ili kuendelea kuwatumikia wananchi.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Sara Yohana amesema pikipiki hizo ambazo watendaji wamekabidhiwa zimenunuliwa kutokana na mapato ya ndani ambapo amewetaka watendaji hao kuzitumia katika shughuli za ukusanyaji wa mapato na kazi nyingine za kiutendaji katika maeneo yao.

Bi Sara Yohana Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wa pili kushoto akisoma taarifa ya awali kwa watumishi wa Halmashauri na watendaji wa kata wakati wa kukabidhi pikipiki 23 zilizotolewa kwa Watendaji wa kata Leo Januari 5, 2024.


“Jumla ya Pikipiki zilizokabidhiwa ni 23  zenye thamani ya shilingi 72,709,100 kutoka mapato ya ndani, awali zilitolewa pikipiki 9 ambazo zilitoka serikali kuu na tayari watendaji walishapewa hivyo halmashauri katika bajeti zake itatenga kiasi kingine cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki 5 ili kukamilisha jumla ya pikipiki 37.” Alisema Kaimu Mkurugenzi

Akitoa shukrani kwa niaba ya watendaji wa kata ndugu Lusekelo Mwaikanda ambaye ni mtendaji wa kata ya Nyarugusu ameishukuru ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita  kwa kuwawezesha watendaji wa kata kupata pikipiki hizo ili ziweze kuwasaidia kutekeleza majukumu yao. “Kwa niaba ya watendaji tunashukuru kupewa pikipiki hizi na tutazitunza, hazitatumika kwa ajili ya biashara, sisi watendaji ni nguvu ya Taifa” alisema Mwaikando.


Ndugu Lusekelo Mwaikenda Mtendaji wa kata ya Nyarugusu akiwa kwenye Moja ya pikipiki zilizotolewa leo Januari 5, 2024 Kwa Watendaji wa Kata

Zoezi hilo la ugawaji wa pikipiki limeshuhudiwa na Mhe Mbunge wa Jimbo la Busanda Mhandisi Tumaini Magesa ,Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Geita  pamoja Watendaji wa kata za Halmashauri hiyo.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongoza na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi ili kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa wananchi ikiwa ni pamoja na ukamilishwaji wa miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.





Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa