• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAPANDE AWATAKA WAHANDISI KUONGEZA UMAKINI KATIKA KUSIMAMIA MIRADI YA SERIKALI

Posted on: August 11th, 2022

Na Michael Kashinde

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Barnabas Mapande amewataka wahandisi wanaosimamia miradi mbalimbali ya Serikali kuongeza umakini katika usimamizi wa miradi hiyo kwa kudhibiti kasoro mbalimbali zinazoweza kujitokeza ili ubora wa miradi hiyo uendane na thamani halisi ya fedha inayotumika.

Ametoa wito huo Agosti 11 akiwa ameambatana na wajumbe wa kamati ya Siasa Wilaya katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo wajumbe hao wamepongeza hatua za miradi mbalimbali waliyoitembelea katika siku ya kwanza ya ziara hiyo.

Ziara ya wajumbe wa kamati ya Siasa Wilaya imeanzia katika kata  ya Izumacheli kwa kutembelea Mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Sekondari Izumacheli pamoja na mradi wa maji unaosimamiwa na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA).

Aidha baada ya ukaguzi wa Miradi hiyo wajumbe hao wakiongozwa na mwenyekiti Mapande wameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kusogeza huduma hizo za kijamii kwa mara ya kwanza katika maeneo hayo ya kisiwani ambayo yalikuwa yanakabiliwa na uhaba wa maji na ukosefu wa shule kwa muda mrefu, huku akitoa wito kwa RUWASA kumfuatilia kwa karibu Mkandarasi wa maji ili amalize mradi kwa wakati sanjari na kuwasiliana kwa karibu na wadau wanaojitolea katika ujenzi wa shule ya sekondari Izumacheli ili Mradi huo wa madarasa ukamilike.

Majuto Cleophace Baltazari mmoja wa wananchi wa Izumacheli amesema kuwa uwepo wa Shule hiyo umewapunguzia gharama ambazo awali walikuwa wakitumia kuwapangishia vyumba wanafunzi wanaokuwa wanasoma mbali hasa Nkome kwa kuwa hakukuwa na shule ya sekondari kabla katika kisiwa hicho.

Wajumbe hao wametembelea pia Mradi wa Zahanati na nyumba ya watumishi katika kijiji cha Chelameno kata ya Lubanga ambao mpaka sasa umegharimu kiasi cha Tshs.108,263,480/= ambapo licha ya kupongeza ujenzi wa mradi huo Mwenyekiti Mapande ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kumsaidia mtendaji wa kijiji hicho kutoa fedha kwenye akaunti ya kijiji kiasi cha Tshs. 50,000,000/= ili kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo kabla ya kikao cha Halmashauri kuu ya Chama Wilaya.

Aidha ziara hiyo imefika pia katika mradi wa shule mpya ya Nyanza katika kata ya Nzera unaohusisha vyumba 8 vya madarasa, utengenezaji wa meza 320, na viti 320, vyumba ya maabara, (Kemia, Fizikia, na Bailojia), jengo la utawala, Maktaba, ICT, matundu 20 ya vyoo vya wanafunzi na 4 ya walimu na mfumo wa maji.

Mpaka sasa shule mpya ya Nyanza imekamilisha vyumba vya madarasa 8 na majengo mengine yanaendelea na ukamilishaji ambapo wajumbe wa kamati ya Siasa Wilaya wameshauri kuongeza umakini ili miradi inayojengwa kwa gharama kubwa kama hii iwe na ubora unaotakiwa ili kuleta tija kama ilivyokusudiwa.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa