• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAPANDE AWATAKA VIONGOZI MBALIMBALI KUMSAIDIA MHE. RAIS KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: August 12th, 2022

Na. Michael Kashinde

Mwenyekiti wa kamati ya Siasa Wilaya ya Geita Barnabas Mapande ametoa wito kwa viongozi mbalimbali kumsaidia Mhe. Rais Samia, kwa kusimamia vizuri fedha zinazokuja kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo ili dhamira yake ya kuleta maendeleo ionekane kwenye jamii.Mapande ametoa wito huo Agosti 12, 2022 alipoambatana na wajumbe wa kamati ya Siasa Wilaya ya Geita na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali katika ziara ya siku ya pili ya ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita  akiwa katika shule mpya ya Mama Samia Katoro inayojengwa kwa Gharama ya Tshs. 600,000,000/= kupitia Mradi wa SEQUIP.

Mapande amepongeza usimamizi mzuri wa ujenzi wa mradi huo ambao hauna kasoro, huku akiendelea kutoa wito kwa Wahandisi wanaopewa dhamana ya kusimamia miradi mbalimbali kuwaelekeza mafundi viwango vya miradi ya Serikali, ili kujenga miradi yenye ubora na itakayodumu muda mrefu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuleta miradi mingi katika Wilaya ya Geita, sambamba na wananchi ambao wamepokea vizuri miradi hiyo na kushiriki kwa kujitolea katika hatua mbalimbali kama vile kuchimba mawe ya msingi na kuleta maji huku akiendelea kuwasisitia wasimamizi wa miradi hiyo kuwaongoza mafundi muda wote ili kuepuka kazi kuharibika.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Busanda Mhe. Tumaini Magesa amewataka wananchi kujiandaa na miradi mbalimbali inayokuja ukiwemo mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Stamico hadi Ushirombo, ujenzi wa Chuo cha VETA katika jimbo la Busanda na kusambazwa kwa umeme katika vijiji vyote vya Busanda kwa Gharama ya shilingi bilioni 25 huku akikishukuru chama chake cha CCM kwa namna kinavyosimamia miradi ya maendeleo.

Mhe. Khadija Said ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ameshukuru kwa ushauri mzuri wanaoupata kutoka kwa viongozi mbalimbali wa chama na Serikali akiahidi kuufanyia kazi huku akishukuru pia kwa Mradi wa shule mpya hiyo ya Mama Samia ambayo anaamini itawahamasisha wanafunzi wengi hasa wa kike kuwa kama Rais wao Mama Samia.

Shule ya Sekondari Katoro imekasimishwa usimamizi wa ujenzi wa shule mpya hiyo ya Mama Samia na kuratibu matumizi ya fedha za mradi huo unaohusisha jengo la utawala, vyumba 8 vya madarasa, maktaba, chumba cha TEHAMA, maabara za kemia, fizikia, na matundu 20 ya  vyoo na Tenki la juu la maji.

Agosti 11 na 12 Kamati ya Siasa Wilaya ya Geita imetembelea miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita iliyoanza kutekelezwa kuanzia mwezi januari mwaka huu ikiwa ni ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na kushauri mambo mbalimbali kulingana na namna wajumbe wa kamati walivyoona miradi hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa