• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAPANDE AWATAKA VIONGOZI KUWAHAMASISHA MAKUNDI YA WAENDESHA BODABODA NA BAJAJI KUKATA BIMA ZA AFYA

Posted on: September 9th, 2022

Na Michael Kashinde

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Ndg. Barnabas Mapande ametoa ushauri kwa viongozi Wilayani Geita kuyafikia makundi mbalimbali katika jamii wakiwemo vijana wa bodaboda na waendesha bajaji na kuyahamasisha makundi hayo kujiunga na mifuko ya Bima za Afya.

Septemba 8, 2022 akiwa katika mkutano wa siku ya pili wa baraza la madiwani kwa kipindi cha robo ya nne kati ya Aprili hadi Juni 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mapande amesema kuwa vijana hao wanatakiwa kukata Bima za Afya yao suala linaloweza kuwasaidia kupata matibabu mazuri hata ikitokea mhusika amepata ajali na akawa hana fedha.

Ametoa wito kwa Halmashauri zinapokuwa zinawawezesha vijana hao kwa kuwapatia mikopo ya makundi maalumu, kuangalia namna nzuri ya kuwahamasisha vijana hao kujiunga katika mifuko ya Bima za Afya ambapo kuna utaratibu rahisi kwa makundi kama hayo kujiunga kwa kuchangia kiasi kidogo.

Ametumia nafasi hiyo kuiomba Halmashauri kuangalia namna ya kutatua changamoto mbalimbali wanazokutana nazo  baadhi ya watu kwa kuambiwa Bima zao hazitumiki suala ambalo kwa sasa halitarajiwi kuendelea kujitokeza, kwa kuwa tayari fedha zilizotolewa na wanufaika wa Bima hizo zimekwishapelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya tayari kwa ajili ya kuwahudumia wanufaika hao.

Aidha Mapande ametumia nafasi hiyo pia kuwataka watumishi wa NIDA Wilayani Geita kuangalia namna ya kuwasaidia kwa haraka baadhi ya wananchi ambao mpaka sasa bado hawajapata vitambulisho wala namba zao za NIDA.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu amewashukuru viongozi wa ngazi mbalimbali kwa namna waliyohamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya watu na makazi ambalo limekamilika kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuhesabu kaya 194,064 sawa na Asilimia 142 ya makadirio ya kufikia kaya 136,388, huku nyumba 233,957 sawa na asilimia 158 zikihesabiwa kutoka makadirio ya nyumba 148,000.


Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TIMU YA MENEJIMENTI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YARIDHISHWA NA KASI YA UKAMILISHAJI WA MIRADI

    October 17, 2025
  • GEITA DC KUENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA BOOST YENYE THAMANI YA BILIONI 3.2

    October 09, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NYANG'WALE ATEMBELEA BANDA LA MAONESHO YA MADINI LA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

    September 24, 2025
  • WAUGUZI WA AFYA NA MAAFISA LISHE GEITA DC WAASWA KUEPUKA MIGOGORO MAENEO YA KAZI.

    September 22, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa