• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAFUNZO YA LISHE KWA WAGANGA WAFAWIDHI WA VITUO VYA AFYA NA WARATIBU WA LISHE GEITA DC

Posted on: May 3rd, 2024

Waganga Wafawidhi kutoka vituo vya afya pamoja na Waratibu wa Lishe Halmashauri ya wilaya ya Geita, leo May 3,2024 wamepata mafunzo kuwajengea uwezo katika maswala ya Lishe.


Awali akifungua mafunzo hayo, Dkt Esideri Nyandoto ambaye ni mratibu wa kinywa na meno Halmashauri ya wilaya ya Geita amewataka wataalam hao kuzingatia mafunzo hayo pamoja na utoaji wa taarifa sahihi katika majukumu ambayo wanatakiwa kuyatolea taarifa ikiwa ni pamoja na changamoto wanazokutana nazo katika maeneo yao ya kazi.


Mafunzo hayo yametolewa na na maafisa lishe wa Halmashauri ya wilaya ya Geita ili kuendelea kukabiliana na tatizo la utapiamlo unaotokana na lishe duni inayopelekea udumavu kwa watoto.


Akizungumza katika mafunzo hayo, Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita bi Ummy Kileo amesema upo Muongozo mpya wa makundi ya vyakula ambapo amesema kwa sasa makundi yapo sita na sio matano. Ummy ameyataja makundi hayo kuwa ni kundi la Nafaka, mizizi yenye wanga ndizi za kupikwa, kundi la mboga mboga, kundi la matunda, kundi la jamii ya kunde, karanga na mbegu zenye mafuta, kundi la vyakula vyenye asili ya wanyama na kundi la mwisho ni kundi la mafuta ambayo ni salama kwa afya.

Muuguzi Kiongozi Hospital ya Wilaya Nzera, Beatrice Munisi amewataka waganga Wafawidhi na maafisa lishe wa vituo vya afya kuwa huduma zenye utu, staa na Heshima katika kutoa huduma huku akiwataka kuwa na mahusiano mazuri ya kuheshimiana nakupenda katika kufanya kazi ili wateja waendelee kupata Huduma Bora.

Aidha katika mafunzo hayo, wataalam hao wamejifunza namna ya kufanya utambuzi wa watoto wenye utapiamlo wa kadiri na mkali kwa kutumia vigezo vya shirika la Afya duniani (WHO) ambapo imeelezwa kwa mujibu wa vigezo vya shirika la Afya duniani (WHO) utapiamlo wa kadiri kwa watoto unamaanisha uwiano wa uzito kwa urefu kati ya Z-alama (mstari wa ukuaji)-3 na <-2 (bila kivimba mwili) , au mzingo wa kati wa sehemu ya juu ya mkono chini ya sentimeta 12.5 lakini ni sawa au zaidi ya sentimeta 11.5.


Kwa upande wa utapiamlo mkali kwa watoto wenye umri kuanzia miezi 6 hadi 59 hutokanana na lishe duni inayojidhihirisha kwa ukondefu mkali wa mwili , ambapo uwiano wa Uzito kwa urefu/kimo upo chini ya Z-score-3 kwenye mstari wa ukuaji au kuvimba kwa miguu yote miwili, au mzingo wa kati wa sehemu ya juu ya mkono chini ya sentimeta 11.5.


Katika mafunzo hayo, Waganga Wafawidhi pamoja na Waratibu wa Lishe katika vituo vya afya ndani ya Halmashauri wametakiwa kuwaelemisha wazazi na walezi wa watoto kula vyakula mchanganyiko kutoka makundi sita ya chakula kila siku kwa na kuzingatia tofauti za vyakula ndani ya kila kundi ili kuzuia utapiamlo na kupunguza hatari ya kupata magonjwa sugu yasiyoambukizwa.

Dkt Jumanne Enos akitoa mafunzo kwa waganga Wafawidhi na Maafisa lishe kutoka vituo vya afya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo amewataka waganga hao na maafisa Lishe kuwashauri wamama wanapojifungua kupata vyakula vya Lishe ili kutengeneza maziwa mengi kwa ajili ya watoto.

Pamoja na hayo, wametakiwa kutoa elimu kwa wazazi na walezi wanao fika kwenye vituo vya afya kuhakikisha wanazingatia usafi wa mazingira katika maeneo wanavyoishi na Usalama wa chakula na maji ikiwa ni pamoja na kuepuka tabia hatarishi za matumizi ya sigara, tumbaku na unywaji wa pombe ili kupunguza hatari ya kupata magonjwa kwa kuwa na mtindo bora wa maisha.


Mafunzo hayo yamehudhuriwa na Waratibu wa Huduma za mama na mtoto, Wauguzi na maafisa lishe ndani ya Halmashauri ambapo kwa nyakati tofauti wamewataka washiriki wa mafunzo hayo kufikisha elimu katika ngazi zote katika vituo vyao vya kazi ili kuendelea kuwajengea uwezo katika kukabiliana na maswala ya Lishe.A


Halmashauri ya Wilaya ya Geita imepokea jumla ya kiasi cha Shilingi milioni 204 kwa ajili ya huduma za afua za lishe katika vituo 57 vya kutoa huduma za Afya.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa