• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAFUNZO KWA MADIWANI WA GEITA KUIMARISHA UONGOZI, MIRADI NA MAPATO YA HALMASHAURI

Posted on: January 29th, 2025

Dodoma, Januari 29, 2025 – Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wamehudhuria mafunzo maalum kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI) Hombolo, Dodoma, kwa lengo la kuboresha utendaji wao katika halmashauri. Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku mbili, Januari 29 na 30, 2025, katika ukumbi wa African Dream Hotel, yakiratibiwa na wawezeshaji kutoka LGTI.

Madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa katika mafunzo.

Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Charles Kazungu, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndugu Karia Magaro. Akifungua rasmi mafunzo hayo, Mhe. Kazungu alisisitiza umuhimu wa madiwani kuwa na uelewa wa kina kuhusu uongozi bora, usimamizi wa fedha, na uendeshaji wa vikao kwa ufanisi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu, akizungumza na madiwani, katika ufunguzi wa mafunzo kwa madiwani yanayoendelea Dodoma.

Naibu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Tafiti na Ushauri Elekezi, Prof. Magreth Bushesha, aliwahimiza madiwani kutumia mafunzo hayo kuboresha utendaji wa halmashauri zao. "Kuna mambo madogo kama uendeshaji wa vikao, ubunifu wa miradi, na usimamizi wa maendeleo ya jamii, ambayo yanaweza kuonekana yasiyo na uzito, lakini yanaathiri sana utendaji wa halmashauri. Ni muhimu kuyafahamu na kuyasimamia kwa ufanisi," alisema Prof. Bushesha.

Naibu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Tafiti na Ushauri Elekezi, Prof. Magreth Bushesha, akizungumza na Madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika mafunzo yanayoendelea Dodoma.

Kwa upande wake, Dkt. Rogers Rugeiyamu, mhadhiri na mwezeshaji wa mafunzo, alibainisha kuwa mafunzo hayo yanalenga kuongeza tija katika halmashauri kwa kuimarisha usimamizi wa fedha na ubunifu wa vyanzo vya mapato. "Mafunzo haya yataisaidia halmashauri kuwa na mipango mizuri ya maendeleo na kujitegemea kifedha," alisema Rugeiyamu.

CPA Charles Matekele, mhadhiri wa fedha na uhasibu kutoka LGTI, alisema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha madiwani kuimarisha usimamizi wa fedha, kuhakikisha matumizi sahihi ya rasilimali, na kupunguza hoja za kikaguzi zinazotokana na kutofuata sheria, kanuni, na taratibu.

Dkt. Rogers Rugeiyamu, mhadhiri na mwezeshaji wa mafunzo akifundisha mada katika mafunzo yanayofanyika Dodoma

CPA Charles Matekele, mhadhiri wa fedha na uhasibu kutoka LGTI akifundisha mada katika mafunzo yanayofanyika jijini Dodoma

Kwa upande mwengine , Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndg. Karia Magaro, alitoa wito kwa madiwani kuzingatia mafunzo hayo na kuyatumia kwa vitendo. "Lazima tuhimize utaratibu wa vikao wenye tija, tuongeze mapato ya halmashauri, na kubuni miradi ya maendeleo ili kutoa huduma bora kwa wananchi wetu," alisema Magaro.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndg. Karia Magaro akizungumza jambo wakati wa uchangiaji baada ya mada, katika mafunzo yanayofanyika Dodoma

Madiwani walioshiriki mafunzo hayo walielezea manufaa yake kwa utendaji wao. Diwani wa Kata ya Ludete, Mhe. Maumuna Bulilo, alisema kuwa amejifunza mbinu mpya za kuendesha vikao kwa muda mfupi lakini kwa ufanisi zaidi. "Awali tulikuwa tukikaa vikao kwa muda mrefu, lakini sasa tumejifunza namna ya kumaliza kikao kwa saa mbili pekee bila kupoteza muda," alisema Bulilo.

Naye Diwani wa Kata ya Bukoli, Mhe. Faraj Seif, alieleza kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuboresha uendeshaji wa baraza la halmashauri, usimamizi wa fedha, uibuaji wa miradi, na ushirikiano na wananchi.

Akihitimisha mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Charles Kazungu, alitoa wito kwa madiwani kuyatumia mafunzo hayo kwa maendeleo ya halmashauri na jamii kwa ujumla. "Mafunzo haya yakalete chanya si tu kwa halmashauri lakini pia kwa jamii tunayoiongoza. Yakalete chanya katika usimamizi wa miradi, usimamizi wa fedha, na pia katika kuelimisha wananchi namna ya kulipa kodi pamoja na tozo za halmashauri ili halmashauri iweze kuendeshwa kwa ufanisi," alisema Kazungu.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa