• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WAASWA KUWA NA LUGHA MOJA KWA AJILI YA MAENDELEO-GEITA DC

Posted on: November 29th, 2023

Na Hendrick Msangi

Madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita sambamba na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashuri hiyo wamefanya ziara katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Novemba 23, lengo kuu ikiwa ni kujifunza namna ya uendeshaji wa shughuli  za maendeleo  na kubadilishana uzoefu katika utendaji.

Awali akiwakaribisha Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama ndugu Clemence Mkuja aliwaeleza Waheshiwa Madiwani na Wakuu wa Idara na Vitengo namna ambavyo Manispaa hiyo inaendesha shughuli zake na kupata mafanikio makubwa katika miradi ambayo inaendelea katika manispaa hiyo ikiwa ni pamoja na utaratibu wa vikao vya baraza kufanyika kwa muda mfupi.

Akiendelea kutoa uzoefu kwa Waheshimiwa Madiwani na Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wa namna wanavyosimamia miradi, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema, Menejimenti inapofanya vizuri katika utekelezaji wa majukumu yao huleta ufanisi mzuri katika utekelezaji wa miradi wanayokuwa nayo. “Menejimenti hukubaliana kufanya miradi michache katika mwaka wa fedha  na kukubaliana na waheshimiwa madiwani kuwa miradi ni kwa ajili ya Manispaa na sio Kata jambo ambalo hupelekea kufanya miradi michache na inayokamilika kwa ufanisi na ubora kwa kuzingatia fedha iliyotengwa” alisema Mkuja.

Pamoja na hayo, Manispaa hiyo huweka vipaumbele vya miradi inayotekelezwa kwa mwaka wa fedha na kuwa na miradi ya kimkakati ambayo hushirikiana na wataalam katika kuiandaa.

Waheshimiwa Madiwani na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakisikiliza namna Manispaa ya Kahama wanavyoendesha Shughulizi za Hospitali ya Manispaa hiyo inayohudumia wagonjwa ndani na nje ya Manispaa hiyo.

Kwa upande wa uwekezaji Manispaa ya Kahama yenye jumla ya kata 20 ,alisema wanatoa ardhi bure kwa wawekezaji  ambapo menejimenti hukaa  na kamati husika kisha hupeleka kwenye baraza la madiwani  na kufanya maamuzi ya pamoja kwa kutoa ardhi bure kwa ajili ya uwekezaji. “Halmashauri ya Manispaa ya Kahama hutoa ardhi bure kwa ajili ya uwekezaji lengo kubwa ni kutengeneza na kuzalisha ajira nyingi kwa wananchi wa Kahama kupitia wawekezaji wanaokuja kuchukua ardhi ambayo hutengwa kwa kuzingatia sheria za ardhi” alisema Kaimu Mkuregenzi huyo.

Madiwani na Wakuu wa Idara wakiwa kwenye Moja ya eneo lililotengwa kwa ajili ya viwanda kwa wawekezaji ambalo limetolewa bure ili kuwavutia wawekezaji kwa ajili ya kuwekeza na kuzalisha ajira nyingi kwa wakazi wa Kahama. 

Sambamba na hilo, Halmashauri hiyo hutoa ajira za muda mfupi katika ukusanyaji wa mapato ikiwa ni pamoja na kuwa na wiki ya ukusanyaji wa mapato ambapo Wakuu wa Idara na Vitengo huingia mtaani kwa ajili ya ukusanyaji wa mapato jambo ambalo limechangia kuongezeka kwa mapato kwenye manispaa hiyo na kuweza kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kuwawezesha wajasiriamali pamoja na kuhamasisha vijana kwenye sekta ya kilimo na kuongeza ajira.

Waheshimiwa Madiwani na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa kwenye moja ya kumbi ndogo za mikutano za Manispaa hiyo ambayo samani zake zimetengenezwa na wajasiriamali wa Manispaa hiyo. Samani zinazotumika kwenye ofisi za Manispaa hiyo hutengenezwa na wajasiramali wa Manispaa hiyo ikiwa ni sehemu ya kuendelea kutengeneza ajira nyingi kwa vijana.

Naye Kaimu Meya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Mzee Hamidu Kapamwa aliwaasa madiwani hao kutokuwa na uadui na watendaji wa halmashauri yao bali kuwa kitu kimoja kwa kufanya kazi kwa kushirikishana , kuheshimiana , kupendana na  kuzungumza  lugha moja na kwenda pamoja ili kuleta maendeleo katika halmashauri yao.

Moja ya Kiwanda cha samani ambacho Manispaa ya Kahama imetoa eneo bure (Ummy Mwalimu Industrial) kwa ajili ya mradi huo ambao zinatengenezwa samani mbalimbali zinazouzwa ndani na nje ya nchi na kuiongezea Manispaa hiyo mapato ya ndani.

Madiwani hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshima Charles Kazungu waliwashukuru wenzao wa Manispaa ya Kahama kwa ukarimu na mapokezi mazuri waliyoyapata na kuwa ahidi kuyafanyia kazi yote waliyojifunza wakishirikana na wataalam ili kuleta maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kutumia uzoefu waliojengewa na wenzao na kuwaomba wazidi kuwa marafiki ili kuendelea kushirikishana namna ya kuendelea kuzijenga Halmashauri ikiwa ni pamoja na usimamizi mzuri wa miradi ambayo serikali inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  inatenga fedha nyingi kwa ajili ya miradi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa