• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAAFISA HABARI NCHINI WAMETAKIWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU UMUHIMU WA KUJIANDIKISHA DAFTARI LA WAPIGA KURA

Posted on: June 15th, 2024

Na Hendrick Msangi

Maafisa Habari nchini wametakiwa kutumia taaluma yao kuelimisha jamii umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya kwanza inayotarajiwa kuanza Julai 1 , 2024.

Akizungumza katika Kikao cha Tume huru ya Uchaguzi na Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri kilichofanyika Ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndugu Ramadhani Kailima amewataka Maafisa Habari wa Serikali Kuwa mabalozi wazuri wa Tume huru ya Uchaguzi kwa kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Mkurugenzi wa Uchaguzi Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ndugu Ramadhani Kailima akizungumza katika Mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Maafisa Habari kutoka Mikoa na Halmashauri nchini Katika Ukumbi wa Mliman City Jijini Dar es Salaam Juni 15,2024.


Hayo yameelezwa Juni 15, 2024 wakati wa Mkutano wa Tume Huru ya Uchaguzi na Maafisa Habari kote nchini.

"Ndugu Maafisa Habari, uboreshaji huu unahusu kila mwananchi mwenye sifa, Tumieni njia mbalimbali kuelimisha jamii umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya kwanza" Amesema Ndg Kailima.

Awali akiwasilisha mada  kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Kwanza, Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura  Bi. Giveness Aswile amesema zoezi hilo linatarajia kuzinduliwa Julai 01, 2024 katika Mkoa wa Kigoma na kisha kuendelea katika mikoa mingine ya Katavi na Tabora, na kufuatiwa na  Kagera na Geita na kasema zoezi hilo hadi kufika Machi 2025 zoezi hilo linatarajiwa kukamilikana kwa awamu ya kwanza.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga kura Bi.Giveness Aswile akizungumza katika Mkutano huo ambapo amesema Kada ya Maafisa Habari ni muhimu kwa nchi yoyote inayotaka kufanikisha Jambo la aina yoyote .

Pamoja na hayo Bi Givennes amebainisha kuwa baada ya uboreshaji wa daftari hilo inatarajiwa kuwa jumla ya wapiga kura 34,746,638 watakuwa wameandikishwa.

“Katika uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kuzingatia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Daftari linatarajiwa kuwa na wapiga kura 34,746,638 kutoka 29,754,699 ya mwaka 2020 hili ni ongezeko la wapiga kura wapya 5,586,433 sawa na asilimia 18.7,” amesema Bi. Givennes katika Mkutano huo.

Aidha Bi Givennes ameongeza kuwa katika zoezi hilo wapiga kura 4,369,531 wanatarajiwa kuboresha taarifa zao na wapiga kura 594,494 wataondolewa katika Daftari kwa kupoteza sifa za kuwa wapiga kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 10 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na 1 ya mwaka 2024.

Akizungumzia kuhusu mfumo mpya saidizi unaofahamika kama Online Voters Registration System, (OVRS) amesema mfumo huu utawawezesha  wapiga  kura walioandikishwa kuanzisha mchakato wa uboreshaji kwa njia ya mtandao kupitia simu ya mkononi au Kompyuta kubadilisha taarifa au kuhama jimbo au kata au kubadilisha  na kuhama.

Maafisa Habari kutoka Mikoa na Halmashauri nchini Tanzania wakifuatilia mada kuhusu maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga Kura awamu ya kwanza ndani ya Ukumbi wa mikutano wa Mliman City Jijini Dar es Salaam.


Jumla ya vituo 40,126  vya kuandikisha wapiga kura vitatumika katika uboreshaji wa Daftari 2024 ambapo 39,709 vipo Tanzania Bara na  417 vikiwa Zanzibar nakufanya Tume kuwa na ongezeko la vituo  2,312  kulinganisha na vituo 37,814 vilivyotumika mwaka 2019/2020.

Kauli mbiu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania inasema Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni Msingi wa Uchaguzi bora

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa