• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAWAKUMBUKA AKINA MAMA WALIOJIFUNGUA NA WAFUNGWA WANAWAKE

Posted on: March 7th, 2023

Na Michael Kashinde

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Machi 8, kila mwaka Halmashauri ya Wilaya ya Geita imewaunganisha wadau mbalimbali wa masuala ya wanawake, na kushiriki kwa pamoja katika zoezi la kufanya usafi katika kituo cha Afya katoro sambamba na kutoa zawadi mbalimbali kwa akina mama waliojifungua pamoja na wafungwa wanawake katika gereza la Wilaya Geita.

Mazoezi hayo yaliyoratibiwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita yamefanyika Machi 6, 2023 yakiwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo kampuni ya dhahabu ya BUCKREEF, chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Wilaya ya Geita (TALGWU), vikundi mbalimbali vya wanawake na Taasisi zinazojihusisha na haki za wanawake na kupinga ukatili.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi. Enedy Mwanakatwe amewashukuru wadau hao kwa ushiriki wao katika zoezi hilo la usafi na zawadi mbalimbali walizojitolea huku akisema kuwa zawadi hizo zitawasaidia akina Mama hao pamoja na watoto wao.

Zawadi hizo ni pamoja na Sabuni katoni 25, Sukari kilo 160, madaftari(Counter books) boksi 12, sabuni za Detol boksi 2 kutoka Kampuni ya BUCKREEF, huku chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Wilaya ya Geita  (TALGWU) wakitoa Taulo za kike kubwa pisi 174 Taulo kwa ajili ya watoto (Pumpers)Pisi 288 na Gloves boksi 3.

Bi. Amelda Msuya Meneja rasilimali watu katika mgodi wa dhahabu wa BUCKREEF akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo amesema kuwa, wameona ni vyema kushiriki na wanawake katika mwezi huu kwa kuwa na wao kama mgodi wana sera ya kuajiri wanawake wengi kadri wawezavyo ili kuendelea kuwatia moyo wanawake kufanya shughuli za madini  ambapo hapo awali jamii iliamini shughuli za migodini zinafanywa na wanaume pekee jambo ambalo kwa sasa limebadilika.

Kwa upande wake Katibu wa TALGWU mkoa wa Geita Wakili Daud Mhagama amesema kuwa wao kama chama cha wafanyakazi wamejitokeza kuungana na wadau wengine kushiriki katika zoezi hilo ili kuwaunga mkono akina mama katika shughuli zao za maendeleo akiwemo Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mama.

Akizungumza pia baada ya kupokea zawadi mbalimbali zilizotolewa kwa ajili ya wafungwa na mahabusu wanawake, katika gereza la Wilaya ya Geita Mratibu Msaidizi wa Magereza Samwel Evans Juma awashukuru wanawake hao kwa zawadi hizo akisema kuwa hiyo inaonyesha wazi kuwa wafungwa na mahabusu hawajatengwa na jamii na wanapotembelewa na watu wanafurahi  kwa kuona jamii inawajali na kuwathamini.

Siku ya wanawake huadhimishwa duniani kote  Machi 8 kila mwaka ambapo kwa mwaka huu 2023 maadhimisho hayo kwa upande wa Mkoa wa Geita yataadhimishwa kimkoa katika viwanja vya AIC Ludete ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mrtin Shigela.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa