• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KLINIKI YA KERO YATATUA CHANGAMOTO SUGU ZA WANANCHI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

Posted on: March 6th, 2024

Na Hendrick Msangi

Katika kutimiza dhamira ya Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kuwatumikia wananchi kwa kuhakikisha kero zinazowakabili zinapata mwarobaini, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita imeendelea kufanya ziara kwa ajili ya Kusikiliza na Kutatua Kero za Wananchi ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akizungumza na wananchi wa kata mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Geita zikiwemo kata za Katoro,Ludete na Kakubilo, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigella amesema Serikali ya awamu ya sita inafanya kazi kwa kuwajibika kuwafuata wananchi ili kutatua kero ambazo zinawapata. “Serikali ya Dkt Samia Suluhu Hassan ni ya wananchi, hivyo kila mtendaji anawajibu wa kuwatumikia wananchi” alisema Shigella.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigella akitatua kero za wananchi waliofika kwenye Kliniki ya kutatua kero za wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Geita. 

Aidha Shigella aliwataka wananchi hao kuepuka kutoa rushwa kwa watendaji wa ngazi zote pale wanapohitajika kutoa, na iwapo kutakuwa na uhitaji wa kutoa fedha basi kuwe na utaratibu katika maandishi

Kwa upande wa kero zinazohusu maswala ya ardhi, Mhe Shigella aliiagiza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kuchukua hatua za haraka kwa watu wenye viwanja ambavyo wanahitaji kujenga ili kuwa na vibali kuepuka kuja kuvunja nyumba za wananchi. Akitolea mfano mji mdogo wa Katoro ambao unakuwa kwa kasi kutokana na kuwa na wafanyabiashara wengi, Mhe Shigella aliwataka viongozi wa vijiji na vitongoji kusimamia vizuri swala la ujenzi ili mji huo upangike vizuri. “Kila mtu anayetaka kujenga ni vema kushirikisha wataalam kwa ajili ya kuwa na mji uliopangika wananchi wajenge kwa kufuata utaratibu.” Alisema Mhe Shigella

Kuhusu swala la vitambulisho vya NIDA ambavyo vimeonekana kuwa kero kwa watu wengi, Mkuu huyo wa Mkoa aliagiza mamlaka zote zinazohusika katika upatikanaji wa vitambulisho vya NIDA kuweka kambi maeneo ambayo wananchi hawajapata Vitambulisho ili vitambulisho hivyo vipatikane kwa uharaka.

Aidha katika kliniki hiyo wananchi walililamikia jeshi la polisi kwa kuwanyanyasa wananchi wanaobeba magunia ya mkaa kwa kuwatoza kiasi cha shilingi laki mbili ambapo Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoani Geita Kamanda Sofia Jongo alilikemea jambo hilo na kusema askari polisi wote wanajihusisha na maswala ya rushwa watachukuliwa hatua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Sofia Jongo amewataka wananchi Mkoani Geita kujiepusha na vitendo vya rushwa na badala yake watoe taarifa kwa vyombo husika pale wanapotakiwa kufanya hivyo

Pamoja na hayo zipo kero za wafanyabiasha kusumbuana na mwenyekiti wa wafanyabiasha katoro kuhusiana na mikataba ya upangishwaji wa vyumba vya biashara na ulipaji wa mapato ambapo Mkuu wa mkoa aliagiza wafanyabiashara hao kuendelea kulipa Halmashauri kama wapangaji wa Halmashauri.

Kuhusu migogoro kati ya wamiliki wa mashamba ambayo yamegundulika kuwa na miamba ya madini na  wamiliki wa leseni za uchimbaji wa madini kutokutoa asilimia 10 kwa  wamiliki wa mashamba hayo, Mkuu wa Mkoa aliagiza wanaotaka kuchimba madini waelewane na wananchi wanaomiliki ardhi ili kuepuka migogoro.

Kuhusu michango wanayochangishwa wanafunzi shuleni, Mhe Mkuu wa Mkoa aliagiza michango hiyo kufuata kibali maalumu kutoka kwa mkuu wa wilaya ili kuepuka migogoro na kusema watoto wasirudishwe nyumbani na kukosa masomo bali utaratibu ufuatwe.

Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Mkoa wa Geita ambapo walisikilizwa kero zao na kupatiwa ufumbuzi. Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan inawafikia wananchi kwenye maeneo yao kwa ajili ya kutatua changamoto zinazowakabili.

Aidha katika ziara hiyo kuliibuka kero kutoka kwa wananchi kuhusu kituo cha afya kakubilo kukamilika muda mrefu lakini hakitoi huduma hivyo kumlazimu Mbunge wa jimbo la Geita vijijini Mhe Joseph Msukuma kutolea majibu mbele ya wananchi na mkuu wa mkoa.

Kufuatia maombi hayo ya wananchi na mbunge ya kufunguliwa kwa kituo hicho cha afya, Mkuu wa Mkoa Wa Geita Mhe Martin Shigella alimuagiza Mganga Mkuu wa wilaya kukifungua mara moja kituo hicho na kuanza kutoa huduma wakati ukamilishaji wa majengo mengine ukiendelea.

Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Mkoa wa Geita ambapo walisikilizwa kero zao na kupatiwa ufumbuzi. Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan inawafikia wananchi kwenye maeneo yao kwa ajili ya kutatua changamoto zinazowakabili.

Akihitimisha ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa Mhe Martine Shigella aliwashukuru wananchi kwa kujitokeza na kuwasihi kufika kwenye ofisi za umma kwa ajili ya utatuzi wa kero zao kwani ofisi zipo kwa ajili yao ikiwa ni pamoja na kuwapa ushirikiano viongozi wao ili kuleta maendeleo katika maneo yao huku akikemea swala la ukatili kwa watoto, rushwa na kuwasisitiza wananchi hao kutambua kuwa swala la ulinzi na usalama ni jukumu la kila mtu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UBORESHAJIWA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025 WAFIKIA KIKOMO GEITA.

    May 08, 2025
  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa