• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KIWANGO CHA UFAULU MTIHANI DARASA LA SABA CHAONGEZEKA KWA ASILIMIA TANO-GDC

Posted on: January 10th, 2024

Na: Hendrick Msangi

IDARA ya Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Januari 9, 2024 imekutana na Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kujadili taarifa ya tathmini ya matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika mwaka 2023

Matokeo hayo yaliyatangazwa na baraza la mtihani Tanzania (BMT) Novemba 23, 2023 na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Said Mohammed, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilikuwa na jumla ya watahiniwa 23,335 walioshiriki kufanya mtihani huo na kushika nafasi ya 5 kati ya Halmashauri 6 za Mkoa wa Geita katika ufaulu wa watahiniwa waliofanya mtihani huo wa upimaji darasa la saba 2023.

Jumla ya shule zilizofanya mtihani huo kwa Halmashauri ya wilaya ya Geita zilikuwa 201 zikiwemo shule 5  za watu binafsi na mashirika ya dini ambapo kiwango cha ufaulu  kwa mwaka 2023 ni asilimia 69.65 hii ikiwa ni ongezeko la asilimia 5.1 za ufaulu kulinganisha na mwaka 2022 ambapo kiwango cha ufaulu kilikuwa asilimia 64.48.

Akizungumza katika kikao hicho cha kujadili taarifa ya tathmini ya matokeo ya mtihani huo wa upimaji katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, Kaimu Mkuu wa Divisheni Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mwl Paul Richard Magubiki amezipongeza kata za Ludete, Katoro, Nyarugusu, Nkome na Nyamigota kwa kufanya vizuri kati ya kata 37 za Halmashauri hiyo na kuzitaka kata ambazo hazikufanya vizuri kuongeza juhudi ili kuleta matokeo mazuri kwa mitihani ijayo.

Maafisa Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika kikao cha kujadili taarifa ya tathmini ya matokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika mwaka 2023 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilishika nafasi ya tano katika ufaulu wa mtihani huo kati ya Halmashauri 6 za Mkoa wa Geita

Aidha alieleza lengo la kikao hicho  ni kujadili taarifa ya tathmini ya matokeo ya mtihani wa upimaji darasa la saba uliofanyika Septemba 13 -14 mwaka 2023 na kuweza kuweka mikakati itakayowezesha  kuwa na muelekeo mzuri kwa mwaka 2024.

Pamoja na hayo Afisa Elimu huyo aliwaeleza Maafisa Elimu kata  kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Imedhamiria kupandisha kiwango cha ufaulu kutoka asilimia 69.65 ya mwaka 2023 hadi kufikia asilimia 85 kwa mwaka 2024 ambapo alisema ni vema kila kata kusimamia mikakati waliyojiwekeaa ili kuongeza  kiwango cha ufaulu . “Mkawahimize Walimu Wakuu kuwasimamia walimu  kufundisha na kufika kazini kwa wakati kwa kuendelea kuwakumbusha sheria na taratibu za utumishi ili tuweze kuitimiza kauli mbiu yetu ya Usimamizi na ufuatiliaji katika sekta ya elimu huleta matokeo chanya na  halisia” alisema Magubiki.

Aliendelea kuwaeleza Maafisa Elimu kata hao kuendelea kuhimiza swala la lishe kwa wanafunzi wawapo shuleni na kuzitaka kamati za lishe kuwajibika kwani mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa ambayo haikufanya vizuri kwenye afua za lishe. Pia Afisa Elimu huyo aliwataka Maafisa Elimu kata hao  kuwafuatilia wazazi wa wanafunzi  watoro ili kuwachukulia hatua  hii ni pamoja na kuchukua  hatua za kinidhamu kwa walimu  wasiotimiza  wajibu wao.

Maafisa Elimu kutoka kata 37 za Halmashauri ya Wilaya ya Geita  wakiwa kwenye kikao cha kujadili taarifa ya tathmini ya matokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika Septemba 13-14, 2023 ambapo kwa pamoja waliazimia kuweka bidii katika Usimamizi na ufuatiliaji katika sekta ya elimu ili kuleta matokeo chanya na halisia.

Jumla ya Wanafunzi 16,148 wamejiunga na elimu ya sekondari kwa mwaka wa masomo 2024 ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kumekuwa na ongezeko la shule 2 za sekondari zilizojengwa kwa fedha kiasi cha shilingi 1,168,560,056 kutoka fedha za wadau wa maendeleo kupitia serikali kuu (SEQUIP).

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi za miradi ya shule zenye ubora kwa ajili ya wanafunzi wanaoendelea kufaulu na kujiunga na masomo ya elimu ya sekondari.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa