• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KATIBU WA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA GEITA KOMREDI MSUYA APONGEZA BARAZA LA MADIWANI USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: August 6th, 2024

Baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Agosti 6, 2024 limefanya Mkutano wake wa kawaida katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa lengo la kuwasilisha taarifa juu ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ngazi ya kata katika robo ya nne Aprili hadi Juni 2024 kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa kata zote 37 za Halmashauri.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu(kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji Ndg Karia Magaro wakati wa Kikao cha baraza la Madiwani 

Akizungumza kwenye Baraza hilo Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Mhe. Charles Kazungu amewataka Watendaji wa vijiji kufafanua kwa undani zaidi juu ya miradi mipya ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Kata zao na kueleza hatua gani miradi hiyo imefikia pamoja na kuzingatia namna nzuri ya uandikaji wa taarifa wanazowasilisha.

Cde Michael Msuya Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Geita amawasihi madiwani kuendelea kusimamia vema suala la ulinzi na usalama katika maeneo yao.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita Cde Michael Msuya  amelipongeza baraza la madiwani  kwa namna ambavyo wanasimamia miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na watumishi wa halmashauri wanavyofanya kazi  kwa weledi kuhakikisha dhamira ya Mhe Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuwatumikia wananchi inatimia.

Waheshimiwa Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa katika Kikao cha baraza la madiwani ukumbi wa Halmashauri ambapo wamewasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ngazi ya kata.

Pamoja na hayo Cde Msuya ameitaka Halmashauri kupitia idara ya Elimu kutumia mapato ya ndani ili kuendelea kuajiri walimu wa muda kwa masomo ya sayansi wakiwemo wa walimu wa kike wakati wakiendelea kusubiri serikali inapoendelea na mchakato wa kuongeza ikama ya walimu.

Vilevile, Cde Msuya amekemea tabia ya utoro wa watoto mashuleni unaopelekea kushuka kwa ufaulu na kuwataka watendaji kuendelea kusaidia kupunguza utoro mashuleni.

Mbali na hivyo Cde Msuya amawasihi madiwani kuendelea kusimamia vema suala la ulinzi na usalama katika maeneo yao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Magaro amelieleza Baraza hilo kuwa Menejimenti itaendelea kufanya utekelezaji wa yote yaliyowasilishwa kwa ajili ya mustakabali wa Halmashauri.

Waheshimiwa Madiwani wakiwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ngazi ya kata katika kikao cha baraza la madiwani Agosti 6,2024.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa