• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KATIBU MKUU WA CCM ASIKILIZA NA KUTATUA KERO 108 ZA WANANCHI

Posted on: August 13th, 2024

Katoro, Geita - Agosti 12, 2024

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameongoza mkutano wa hadhara katika viwanja vya CCM Katoro, Wilayani Geita, ambapo amesikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi. Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwemo Naibu Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Dotto Biteko, na Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Nchemba.

Dkt. Nchimbi amepokea kero 108 kutoka kwa wananchi 61 na kutoa ufumbuzi wa kero hizo, huku baadhi zikikabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhe Martin Shigela, kwa hatua zaidi.

Balozi Dkt. Nchimbi Katibu Mkuu Chama cha Mapinduzi (CCM) amepokea kero 108 kutoka kwa wananchi 61 na kutoa ufumbuzi wa kero hizo, huku baadhi zikikabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhe Martin Shigela, kwa hatua zaidi.

Wabunge wa wilaya ya Geita , Mhe. Tumaini Magesa (Jimbo la Busanda) na Mhe. Joseph Musukuma (Jimbo la Geita vijijini), wamepongeza juhudi za Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kufanikisha miradi ya maendeleo, huku wakitoa wito wa kuundwa kwa Halmashauri ya Mamlaka ya mji mdogo wa  Katoro kutokana na ongezeko la wakazi na shughuli za kiuchumi.

Mbunge wa Jimbo la Geita vijijini Mhe Joseph Musukuma ameeleza  hofu ya wafanyabiashara kuhusu mamlaka ya mapato na kumuomba Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kukaa na Mamlaka ya mapato Tanzania ( TRA) na wafanyabiashara kwani kuna tatizo

Kwa upande wake Mbunge Musukuma alieleza hofu ya wafanyabiashara kuhusu mamlaka ya mapato, akisema, "Nikuombe Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wakae TRA na wafanyabiashara kwani kuna tatizo, ni vyema mkutane na kujadili ili kufikia maelewano." Mbunge huyo pia alisisitiza umuhimu wa kutatua tatizo la gharama kubwa za mabango ya biashara katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro.

Wananchi Mkoa wa Geita wakiwa katika viwanja vya CCM-Mamlaka ya Mji mdogo wa Katoro walipofika kumsikiliza Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi katika mkutano wa hadhara Agosti 12,2024 ambapo kero mbalimbali zilitatuliwa.

Naye Naibu Waziri wa Ujenzi alitangaza kuwa barabara ya Katoro kwenda Ushirombo yenye urefu wa kilomita 39 itaingia katika ujenzi wa kiwango cha lami mwaka huu, huku hatua za manunuzi na mazungumzo na mkandarasi zikiwa zimeanza. Pia, alibainisha kuwa barabara inayounganisha Geita na Shinyanga kupitia Mtakuja na Nyarugusu imeanza kutangazwa kwa mkandarasi ambapo zitasaidia shughuli za kiuchumi katika mikoa hiyo.

Katika jitihada za kuimarisha usalama, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Daniel Bassil Sillo ametoa wito kwa mamlaka wa kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi na kuahidi kujenga kituo cha polisi cha kisasa kwa mji wa Katoro. "Anzisheni vikundi vya ulinzi shirikishi na toeni taarifa kwa polisi ili kuchukua hatua. Msiwafuge wahalifu,"amesema Naibu Waziri.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, ameagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuitisha kikao cha wafanyabiashara wa Katoro ili kujadili kero zao na kuboresha mazingira ya biashara,huku Waziri wa fedha Dkt. Nchemba, akisisitiza kuwa serikali imechukua hatua madhubuti kushughulikia kero za kodi na wafanyabiashara. "Namuelekeza Meneja wa Mapato pamoja na wakurugenzi kushughulikia kero hizi. Rais ameunda kamati maalum kushughulikia mambo haya, na itaendelea kufanya kazi kuhakikisha mambo yanaenda vizuri," amesema Dkt. Nchemba.

Katika Mkutano huo Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Dotto Biteko, amesifu mfumo wa kidigitali wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ukusanyaji wa kero za wananchi,  "CCM inafanya kazi yake kisayansi, Ukusanyaji wa kero kwa njia ya kidigitali unasaidia kufanya tathimini na kujua kero ngapi zimeshughulikiwa, na ni wangapi wamehusishwa. hatua hii ni muhimu katika utekelezaji wa ilani ya chama na kuimarisha uhai wa chama."amesema Mhe Biteko.

Viongozi mbalimbali wakihutubia katika mkutano wa Katibu Mkuu Chama cha Mapinduzi uliofanyika katika viwanja vya CCM-Katoro Agosti 12, 2024


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa