• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA MWENGE WA UHURU MKOA YAKAGUA MAENDELEO YA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU

Posted on: September 10th, 2024

Kamati ya Mwenge wa Uhuru ya Mkoa wa Geita imefanya ukaguzi wa miradi mbalimbali inayohusiana na maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru, unaotarajiwa kupokelewa Oktoba 5, 2024, katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Ziara hiyo imefanyika leo, Septemba 10, 2024, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Mwenge wa Mkoa ambaye pia ni Kaimu Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Geita, Eliphas Misenya. Kamati hiyo imeambatana na Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Alex Helman, pamoja na wataalamu kutoka ngazi ya mkoa na halmashauri.

Katika ziara hiyo, Kamati imetembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa sita katika Shule ya Sekondari ya Kasota. Kamati imefurahishwa na hatua iliyofikiwa, ikielezea matumaini makubwa ya kukamilika kwa mradi huo kwa wakati.

Mradi wa vyumba sita vya madarasa katika shule ya Sekondari Kasota.

Vilevile, Kamati hiyo imetembelea shamba la miti lililopo Kata ya Igate na kujiridhisha na matunzo bora ya shamba hilo, na kutoa pongezi kwa juhudi zinazofanywa kulihifadhi.

Mradi wa miti katika kata ya Igate.

Katika ziara ya Ofisi ya Kata ya Nzera, Mwenyekiti wa Kamati Eliphas Misenya amepongeza maendeleo ya ujenzi wa ofisi hiyo, akibainisha kuwa ushauri walioutoa awali umetekelezwa kwa ufanisi.

Mradi wa ujenzi wa ofisi ya kata ya Nzera, uliopo kata ya Nzera.

Kamati pia imetembelea ujenzi wa barabara ya lami nyepesi yenye urefu wa kilomita 1.1, ambayo inatarajiwa kuwekwa jiwe la msingi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru. Mhandisi wa TANROADS Mkoa wa Geita, Jonas Malugu, amepongeza hatua ya ujenzi wa barabara pamoja na maendeleo ya ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Nzera, ambayo imefikia hatua za mwisho.

Mradi wa ujenzi wa Barabara ya lami nyepesi yenye urefu wa Kilomita 1.1 uliopo katika kata ya Nzera

Aidha, Kamati imekagua maendeleo ya kituo cha afya kilichoboreshwa kutoka Zahanati ya Nkome na sasa kikiwa na huduma za kina mama na watoto pamoja na jengo la maabara. Mganga mfawidhi wa Zahanati hiyo, Charles Kaflela, ameweka wazi kuwa kituo hicho kilichoboreshwa kitakuwa na uwezo wa kuhudumia zaidi ya watu 3,000 kwa mwezi, ikilinganishwa na zaidi ya watu 1,800 waliokuwa wakihudumiwa hapo awali. Kituo hicho kinatarajiwa kuzinduliwa rasmi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Oktoba 5, 2024.

Mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Nkome, kilichopo katika kata ya Nkome.

Kamati ya Mwenge wa Uhuru imeeleza kuridhishwa na maendeleo ya miradi iliyokaguliwa na kusisitiza umuhimu wa miradi hiyo kukamilika kwa wakati ili kutimiza malengo ya maendeleo katika Mkoa wa Geita.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MSIRUDISHE WANAFUNZI NYUMBANI KWA SABABU YA MICHANGO – MHE. SHIGELA

    May 24, 2025
  • AFYA, ELIMU, MAJI, KUENDELEA KUPEWA KIPAUMBELE GEITA.

    May 17, 2025
  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa