• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO YA PONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI-GEITA DC

Posted on: July 18th, 2024

Kamati ya fedha, uongozi na mipango  Halmashauri ya Wilaya ya Geita Julai 17 imefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo  inayotekelezwa katika kata mbalimbali za Halmashauri.

Makamu mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni diwani wa kata ya Isulwabutundwe Mhe.Maweda James Gwesandili na mjumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni diwani wa kata ya Rwamgasa Mhe. Kaparatusi Joseph na wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wametembelea na kukagua utekelezaji wa miradi katika shule za Sekondari zilizopo katika  kata za Ludete, Katoro na Nyarugusu.

Kamati ya fedha uongozi na mipango ikikagua ujenzi wa madarasa shule ya sekondari Bugayambelele kata ya ludete ambapo wamepongeza hatua za utekelezaji zilizofikiwa katika mradi huo wenye thamani ya kiasi cha shilingi milioni 214,400,000

Wakiwa kata ya Ludete kamati hiyo imetembelea miradi ya ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa na matundu 8 ya vyoo, iliyopo katika shule za sekondari Bugayambelele na Ludete, zenye zaidi ya wanafunzi 3000.

 Kamati ya fedha uongozi na mipango ikikagua ujenzi wa matundu 8 ya vyoo katika shule ya Sekondari ya  Ludete iliyopo katika kata ya ludete

Miradi hiyo yenye  thamani ya shilingi milioni 214,400,000 utekelezaji wake umekamilika kwa asilimia 97 ambapo Mhe Gwesandili amepongeza hatua iliyofikiwa katika ukamilishaji wa miradi hiyo.

Aidha katika shule ya Sekondari ya Ludete Mhe Gwesandili amepongeza ujenzi wa choo cha wasichana uliozingatia chumba cha kubadilishia taulo za kike pamoja na wanafunzi wenye ulemavu ambapo  kamati hiyo imesisitiza miradi hiyo kuwa na mifumo bora ya maji kabla ya kukabidhiwa ifikapo Julai 30, 2024

Kamati ya fedha uongozi na mipango ikikagua ujenzi wa madarasa katika ziara iliyofanyika Julai 17. Kamati hiyo imewapongeza madiwani na watendaji wa kata pamoja na wakuu wa shule kwa usimamizi mzuri wa miradi inayotekelezwa katika kata hizo

Kwa upande wa Kata ya Katoro kamati imetembelea mradi wa ukarabati wa vyumba vya maabara katika shule ya sekondari ya Samia. Mradi huo umegharimu shilingi Milioni 100 na unategemewa kutumika katika utafiti wa masomo ya Fizikia, Bailojia na Kemia ambapo utahudumia zaidi ya wanafunzi 500.

Ukamilishwaji wa Maabara kwa ajili ya kujifunzia masomo ya Sayansi (Fizikia, Bailojia na Kemia) katika shule ya Sekondari Samia wenye thamani ya  shilingi Milioni 100 ambao utahudumia zaidi ya wanafunzi 500

Pia kamati imekagua mradi wa ujenzi wa vyumba 7 vya madarasa na ukamilishaji wa vyumba 4 vya madarasa katika shule ya Sekondari Lutozo  ambao umekamilika kwa asilimia 98 huku thamani ya mradi ikiwa shilingi Milioni 224,637,700. Mradi huo utakapokamilika unaotarajia kuhudumia zaidi ya wanafunzi 2200

Naye  Mkuu wa Shule ya Sekondari Lutozo Mwl Revocatus Joseph Malaha  ametoa shukrani zake kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia  fedha za miradi  kiasi cha shilingi milioni 381 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa yatakayotumiwa na wanafunzi wa kidato cha  tano na cha sita unaotarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa kutembelea kata ya Nyarugusu na kukagua ujenzi wa bweni la wanafunzi wakike katika shule ya sekondari Evarist unaotekelezwa kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) pamoja na nguvu za wananchi wa kata hiyo. Mradi huo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 180 na upo katika hatua ya boma.

Kamati hiyo imewapongeza madiwani na watendaji wa kata pamoja na wakuu wa shule kwa usimamizi mzuri wa miradi inayotekelezwa katika kata hizo.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuleta fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo ambayo inatekelezwa ndani ya Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa Mkurugenzi Mtendaji ndg Karia Rajabu Magaro.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa