• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA BUNGE INAYOSIMAMIA MAMBO YA AFYA NA MASWALA YA UKIMWI YATEMBELEA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

Posted on: March 15th, 2024

Na Hendrick Msangi:

Kamati ya Bunge inayosimamia mambo ya afya na maswala ya Ukimwi, Machi 15, 2024 imefanya ziara Kata ya Bugulula Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili kuzungumza na wanafunzi pamoja na kuona namna ambavyo wanafunzi hao wamejifunza jinsi ya kupambana na kudhibiti ugonjwa hatari wa Ukimwi.

Awali akisoma taarifa mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge inayosimamia sekta ya afya na maswala ya Ukimwi, Mkurengezi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu Karia Rajabu Magaro amesema jitihada zinafanyika kukabiliana na janga la Ukimwi ambapo jumla ya vituo 53 vya tiba vinatoa huduma rafiki kwa vijana.

Aidha Magaro amesema Halmashauri inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuendeleza juhudi za kuwajengea uwezo wananchi kutambua athari zitokanazo na Ukimwi ikiwa ni pamoja na kuwa tayari kujitokeza kupima, na kuwahimiza kutumia dawa wale ambao wamekutwa na maambukizi ya VVU.

Pamoja na hayo Mkuregenzi Magaro ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kuendelea kutoa fedha, kuweka mazingira wezeshi na kujenga uwezo wa wahusika katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo huku akiutaja Mradi wa Timiza Malengo ambao umetoa mitaji ya kuanzisha biashara  ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita julma ya Kata  37 na vijiji 145 zimenufaika na mradi huo ambapo shilingi 146,575,700 zilipokelewa huku jumla ya mabinti  571 wakinufaika kila mmoja kiasi cha shilingi 256,700 kama mtaji wa biashara.

Wajasiriamali kata ya Bugulula ambao ni wanufaika wa mradi wa Timiza Malengo wakiileza kamati ya Bunge inayosimamia sekta ya afya na maswala ya Ukimwi mafanikio waliyoyapata baada ya kuwezeshwa kiasi cha shilingi 250,000 kila mmoja ambapo wamesema kupitia mtaji huo wameweza kuwasomesha watoto, kujenga na kuzihudumia familia zao.

Mradi wa Timiza Malengo  ulianza kutekelezwa na serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita 2022/2023 pamoja na mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali ya AMREF Tanzania pamoja na TAYOA, Ukiratibiwa na ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI-TACAIDS kwa ufadhili wa mfuko wa Dunia (Global Fund)  ambao lengo lake ni  kuwasaidia  wasiachana balehe, na wanawake vijana wenye umri  wa miaka 10 hadi 24 walioko shuleni kuhitimu  elimu  na walio nje  ya mfumo wa elimu  kuwezeshwa  kijamii na kiuchumi ili kujikimu  kimaisha wakiwa salama  dhidi ya VVU na UKIMWI.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayosimamia mambo ya afya na maswala ya Ukimwi, Mhe Stanslaus Haroon Nyongo ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki amewataka wanafunzi wa shule ya msingi Bugulula  kutokujamiana ili kuepuka kupata maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi pamoja na magonjwa mengine yanayotokana na ngono zembe pamoja na mimba za utotoni na kuwataka kutoa taarifa kwa walimu au wazazi wao pale wanapoona kuna watu wanawasumbua ikiwa ni pamoja kuwashauri wazazi wao kuwahimiza kutumia dawa wale ambao wamepata maambukizi na kuepuka unyanyapaa kwa wagonjwa wenye maambukizi ya VVU.

Waheshimiwa wabunge kamati ya bunge inayosimamia sekta ya afya na maswala ya ukimwi walipotembelea shule ya Msingi Bugulula kata ya Bugulula iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Geita

“Tumetembelea maeneo mbalimbali kujionea uwekezaji mkubwa unaofanywa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta ya afya na leo tupo Geita Kata ya Bugulula, Mhe Rais anatutaka watanzania wote tuwe na afya bora ndio maana amewekeza kwenye vituo vya afya, kwenye zahanati, hospitali za wilaya,hospitali za Mikoa, Kanda na Hospitali za Rufa, tumepita kuona ni jinsi gani serikali imefanya kazi kubwa katika kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi” Alisema Mhe Nyongo.

Kwa upande wake Mhe Ummy Nderiananga Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu amewataka wanafunzi hao kuendelea kuweka bidii katika masomo yao na kutokuwanyanyapaa waathirika wa maambukizi ya VVU.

Mhe Ummy Nderiananga Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Bugulula ambapo amewata kuepuka unyanyapaa kwa waathirika VVU.

Wakiendelea kuwahusia wanafunzi wa shule ya msingi Bugulula, Mbunge wa jimbo la Mtambwe kaskazini Pemba Mhe Khalifa Mohamed Issa amewata wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili wafanikiwe huku wakilishika somo la Ukimwi kwani Ukimwi bado upo na unaua na kuwataka kuacha unyanyapaa kwa wale ambao wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi ikiwa ni pamoja na kutumia dawa kama wanavyoelekezwa na madaktari.

Kamati hiyo ya Bunge imepita katika shule hiyo ya msingi ya Bugulula kujionea jinsi wanafunzi hao walivyojifunza mbinu mbalimbali za namna ya kupambana ukimwi na ikiwa ni pamoja na kupunguza unyanyapaa.

Pamoja na kutembelea shule ya msingi Bugulula, kamati hiyo iliwetembelea wajasiriamali kata ya Bugulula ambao ni wanufanika wa Mradi wa Timiza Malengo ambao umewawezesha kujikwamua kiuchumi ili kuepuka kufanya kazi ambazo zinaweza kuwa hatarishi na kupelekea kupata maambukizi ya Ukimwi. “Endeleeni kufanya biashara ili msiingie kwenye mazingira hatarishi na kusababisha kupata maambukizi ya vvu” alisema Mhe Nyongo.

Naye Mhe Diwani wa kata ya Bugulula Mhe Lupuga aliishukuru Kamati hiyo na kuiomba kuendelea kuweka nguvu ili kituo cha afya cha Kasota kianze kutoa huduma ya upasuaji kwani kituo hicho kimekamilika vifaa vyote isipokuwa huduma ya upasuaji wa dharura ambapo Halmashauri kupitia ofisi ya Mkuregenzi ilisema bajeti ya ukamilishwaji inaendelea na ifikapo mwezi wanne kituo hicho kitaanza kutoa huduma ya upasuaji.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu akiishukuru kamati ya Bunge kwa kuitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Geita Machi 15,2024 ambapo amesema Wilaya ya Geita itaendelea kuiunga mkono serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kwa niaba ya baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuleta fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi katika miradi ya shule na huduma za afya pamoja na kamati hiyo ya Bunge kwa kuitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa