• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

JAMII YA ASWA KUIPA KIPAUMBELE LISHE YA WATOTO-GEITA DC

Posted on: April 4th, 2024

Na: Hendrick Msangi

MAADHIMISHO ya siku ya Afya na Lishe na Uzinduzi wa chanjo Kiwilaya yamefanyika Aprili 4, 2024 katika kata ya Lwezera na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama, serikali na taasisi za dini pamoja na kuambatana na burudani ya ngoma za asili na nyimbo za burudani.

Akizungumza katika maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Bless Mwakyusa ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na rasilimiali watu Halmashauri ya wilaya ya Geita amewasihi wananchi kuhakikisha maswala ya Lishe ya watoto yanapewa kipaumbele kuanzia majumbani kwenye ngazi ya kaya hadi shuleni.

Mhe Chinchina ambaye ni Diwani wa Kata ya Lwezera akiwa na Maafisa na wadau mbalimbali pamoja na Watoto waliojitokeza kwenye siku ya maadhimisho ya siku ya afya na lishe na uzinduzi wa chanjo wakinywa uji wenye virutubisho ambao uliandaliwa na wazazi waliopewa semina elekezi ya namna ya kuandaa uji huo katika maadhimisho ya sikuya afya na lishe na uzinduzi wa chanjo

Akiendelea kuzungumza katika ufunguzi wa maadhimisho hayo, Bi Bless amewataka watumishi wote wa idara ya afya na Lishe kuendelea kutoa ushirikiano kwa jamii katika maswala ya lishe.

“Mkashirikiane na Idara mtambuka, wadau wa maendeleo na wananchi wote kwa ujumla kuhakikisha maswala ya lishe yanapewa kipaumbele kwani  lishe ni suala mtambuka linalohusisha wadau wote na wananchi hasa katika muktadha mzima wa kubadili tabia ya ulaji wa vyakula unaozingatia misingi ya lishe.”alisema Bi Bless Mwakyusa.

Wananchi wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu Bi Bless Mwakyusa wakati wa maadhimisho ya siku ya afya na lishena uzinduzi wa chanjo.  

Pamoja na hayo bi Bless amesema Lishe duni hupelekea kuhatarisha ufaulu wa watoto wanapofikia umri wa kwenda shule, pamoja na kuathiri ustawi wa kimwili na utendaji wa kiaikili kwa watoto ikiwa ni pamoja na kuleta athari katika afya ya uzazi mambo ambayo hutokana na uelewa hafifu  juu  ya  ulishaji wa vyakula sahihi kwa watoto na ambao hauzingatii makundi 6 ya chakula.

Bi Bless amewataka wazazi na walezi kuweka mikakati itakayoweza kuboresha lishe kwa watoto ikiwa ni pamoja na kuwanyonyesha watoto kwa kipindi cha miezi 6 na pindi watakapo maliza miezi 6 walishwe chakula mchanganyiko.

Afisa Utumishi huyo  amewasihi wazazi kuwapa watoto mlo kamili na  salama  na kuwataka kuadhimisha siku ya  afya  na lishe kwa kila kijiji kila robo ya  mwaka pamoja na kutoa elimu ya afua za lishe ili kuendelea kukabiliana na utapiamlo na udumavu ndani ya jamii na kuhakikisha inakuwa salama na yenye afya bora

Naye Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Nasim Ginga amesema lengo la maadhimisho hayo ni kuendelea kuongeza hamasa, kujenga uwezo wa pamoja na kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu faida za lishe bora na madhara ya lishe duni katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Nasim Ginga akimuelezea Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu aina ya vyakula ambayo vinatumika kuandaa lishe bora kwa watoto. 


Kwa upande wake Diwani wa kata ya Lwezera ambapo maadhimisho hayo yamefanyika Mhe Chinchina ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kuendelea kuyatumia maeneo wanayoishi kwa ajili ya kilimo ili kuendelea kupata lishe na kuomba uongozi wa Halmashauri kusogeza huduma za vipimo vya lishe kuepuka kwenda mbali kuvifuata ili kuendelea kuhamasisha wananchi.


Akifunga maadhimisho hayo Bi Bless amesema Serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuendelea kutoa elimu na hamasa ya afua za lishe kuanzia kwenye shule na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo Bi Bless alizitaka kila shule kuhakikisha zinakuwa na viwanja vya michezo kwa ajili ya wanafunzi, kutenga maeneo kwa ajili ya bustani za mbogamboga, miche ya matunda na ufugaji wa wanyama wadogo ili kuendelea kupunguza athari zitokano na lishe duni kwani kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika imebainika Mkoa wa Geita kuwa na idadi kubwa ya watoto walio duma kwa asilimia 38.6.

Maadhimisho hayo yamekuwa  na manufaa  makubwa kwa washiriki na wadau waliohudhuria ambapo wamejifunza namna ya kuandaa uji bora wa lishe kwa ajili ya watoto pamoja na kuwafahamu  wadau na maafisa wanaosimamia  masuala ya afya na lishe.

Msimamizi wa huduma za afya ngazi ya jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Amida Yindi akiwasajili watoto kwenye daftari la Mradi wa Lishe USAID Afya Yangu (RMNCAH). Pamoja na usajili huo wazazi hao walisisitizwa kupatia vyakula vya lishe ikiwa ni pamoja na kuwanyonyesha watoto ambao hawajafikia umri wa kupewa vyakula vya nyongeza.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya sekta ya afya pamoja na kuendelea kuratibu na kusimamia sera zinazohusu masuala ya lishe kama hatua ya kukabiliana na utapiamlo na udumavu ndani ya jamii na kuhakikisha inakuwa salama na yenye afya bora na ustawi ambayo itachangia kikamilifu katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Maafisa Lishe wakiwa katika zoezi la kuwapima watoto katika maadhimisho ya siku ya afya na lishe na uzinduzi wa chanjo yenye kaulimbiu isemayo Lishe Bora ni Msingi wa Maendeleo, SoteTuwajibike.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa