• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU KWENYE UKUSANYAJI WA MAPATO.

Posted on: July 12th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, amesema kuwa ni muhimu kwa Halmashauri kuja na njia mbadala lakini sahihi kwenye shughuli za ukusanyaji wa mapato ili kuongeza mapato kwenye Halmashauri husika pamoja na kufikia malengo ambayo Halmashauri imeweka.

Akizungumza Julai 11 2025, katika ukumbi wa EPZ-Bombambili Manispaa ya Geita kwenye Kikao Kazi cha kujadili tathmini ya mwaka wa fedha 2024/2025 kwa Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya Wilaya pamoja na wa Halmashauri ya Manispaa, Geita, Mhe. Komba ametoa pongezi kwa Wakurugenzi wa Halmashauri hizo kwa kusimamia maelekezo ya Serikali kwenye suala la ukusanyaji wa mapato, uliowezesha uvukaji wa bajeti ulokasimiwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Aidha, Mhe. Komba amesema kuwa, Halmashauri hizo zinapaswa kuongeza ubunifu kwa kujielekeza kwenye miradi mikubwa na ya kimkakati badala ya kutegemea sekta ya madini pekee, pamoja na kutilia mkazo kwenye vyanzo ambavyo vilionyesha kutokufikia lengo kwenye ukusanyaji wa mapato ili kuwe na tija kwenye zoezi hilo.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya, Bi. Lucy Beda, aliagiza Idara za Biashara kutoka Halmashauri zote mbili, kuongeza usimamizi pamoja na ufuatiliaji wa leseni za biashara ili kudhibiti upotevu wa mapato, huku pia akisisistiza suala la uwajibikaji na ufanyaji wa kazi kwa kushirikiana miongoni mwa Idara na Vitengo huskia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Ndg. Karia Magaro, amewataka watumishi kufanya kazi kwa weledi na nidhamu ili lengo la ukusa yaji wa mapato liweze kufikiwa, pamoja na kuziagiza Idara na Vitengo vinayohusika na ukusanyaji wa mapato kuwasilisha taarifa sahihi ya hali ya ukusanyaj kwenye maeneo yao.

Awali wakati akisoma taarifa ya jumla ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri ya Wilaya, Geita, Mwekahazina Bi. Eveline Ntahamba amesema kuwa, ili kufikia lengo la Bilioni 14 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ambalo Halmashauri imejiwekea, Halmashauri imejipanga kuogeza timu ya wakusanya mapato pamoja na kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Kikosi Kazi cha Ukusanyaji wa Mapato.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WASIMAMIWE KUHAKIKISHA AFUA ZA LISHE ZINATEKELEZWA - MHE. KOMBA

    July 12, 2025
  • HALMASHAURI ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU KWENYE UKUSANYAJI WA MAPATO.

    July 12, 2025
  • VIKUNDI 111 VYANUFAIKA NA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA

    July 11, 2025
  • MHE. KOMBA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA OFISI YA KATA, BUGULULA.

    July 05, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa