• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Wilaya ya Geita yatoa mkopo wa milioni 177 kwa vikundi.

Posted on: February 27th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetoa kiasi cha shilingi milioni 177, kwa vikundi vya wanawake, vijana pamoja na watu wenye ulemavu, vyenye jumla ya wanachama 460, kwa kipindi cha robo ya tatu (Januari hadi machi, 2019).

Fedha hizo zimetolewa katika pesa iliyotengwa na Halmashauri  shilingi milioni 330 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi hivyo, katika mwaka 2018/2019 ikiwa ni kutokana na mapato ya ndani asilimia ya 10% ambapo wanawake watapata 4%, vijana 4% na watu wenye ulemavu  2%.

Akizungumza katika zoezi la muendelezo wa kusaini mkataba wa mkopo pamoja na kutoa hundi kwa vikundi hivyo kwa robo ya tatu, Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Geita Donald Nssoko amesema mkopo huo ulianza kutolewa kwa vikundi toka Julai hadi Disemba 2018.

Aidha amesema Halmashauri imetoa muda wa nyongeza wa mwezi mmoja zaidi kwa vikundi kurejesha mikopo, hivyo baada ya kurejesha fedha hizo ndani ya kipindi cha miezi 3, watarejesha kwa miezi 4.  

Mratibu Afisa Maendeleo ya Jamii Mathelina Mgina ameongeza kuwa Halmashauri ya Wilaya imeamua kuongeza muda wa kurejesha mkopo huo kwa vikundi,ikiwa ni kuunga mkono sera ya viwanda, kwa kuwa baadhi ya vikundi vinajishughulisha na  viwanda vidogo vidogo hivyo Halmashauri imetoa muda wa ziada ili viweze kufanya maandalizi ya uzalishaji wa bidhaa zao.

Hata hivyo Mgina amesema pamoja na mafanikio ya watu hasa wenye ulemavu kuhamasika kujiunga kwenye vikundi kwa lengo la kujiongezea kipato, lakini bado kuna changamoto ya mwitikio mdogo wa kujiunga kwenye vikundi kwa baadhi ya vijana wa bodaboda,wavuvi pamoja na wachimbaji madini.

Akiongea kwa niaba ya vikundi mwenyekiti wa kikundi cha Nyarugusu Women Miners Donatha Yakubona, ameishukuru Halmashauri ya Wilaya pamoja na Serikali kwa ujumla kwa kutoa milioni 177 kwa ajili ya kuwawezesha na kuahidi kutumia fedha hizo za mkopo kwa malengo yaliyokusudiwa pia kuzirejesha ndani ya muda uliopangwa.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa