Kwa mwaka wa pili mfululizo, Halmashaur ya Wilaya ya Geita imefanikiwa kupata hati safi kutoka ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, hali iliyochagizwa na usimamizi madhubuti wa fedha za umma, pamoja na ongezeko la mapato ya Halmashauri kutoka bilioni 4 mpaka bilioni 11 kwa mwaka wa fedha 2023/2024.
Akizungumza mapema hii leo, Juni 13 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kujadili taarifa ya majibu ya hoja na mpango kazi wa utekelezaji wa mapendekezo ya taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Kaimu Mkuu wa Mkoan wa Geita ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa ameipongeza Halmashauri kwa kupata hati hiyo, pamoja na kutoa rai kwa Waheshimiwa Madiwani kuendelea kusimamia makusanyo yanayopatikana kwa maslahi ya wananchi kwa ujumla, na hivyo kuinua uchumi wa Halmashauri.
Mhe. Fatma ameongeza kwa kuwataka wataalamu wa uchumi kufanya tathmini ya kina ya vyanzo vya mapato ili viwe na uhalisia wa kiutendaji katika ukusanyaji wa mapato kwa kujumuisha vyanzo vilivyosahaulika au vilivyowekewa makadirio madogo.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa