• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YANUFAIKA NA VIFAA NA SAMANI MBALIMBALI KWA AJILI YA SHULE 5 NA KITUO CHA AFYA KATORO KUTOKA BENKI YA NMB ZENYE THAMANI YA TSHS. MILIONI 30

Posted on: April 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule akiwa katika ziara ya kikazi Aprili 25, 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita amepokea mashuka 30, vitanda 10 na magodoro yake, viti 50, meza 50 pamoja na madawati 50 kutoka Benki ya NMB, vyenye thamani ya shilingi milioni 30 kwa ajili ya shule 5 na kituo cha Afya katoro.

Akipokea vifaa hivyo katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika katika kituo cha Afya Katoro  Mhe. Senyamule ameishukuru Benki hiyo ya NMB kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita katika kuboresha huduma za jamii huku akitoa wito kwa wanafunzi kutambua wajibu wao ni kusoma kwa bidii ili wafaulu vizuri na baadae kuja kulitumikia Taifa katika nafasi mbalimali.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB kanda ya ziwa Bw. Baraka Ladislaus amesema kuwa Benki hiyo imekuwa na utaratibu wa kusaidia huduma za jamii hasa katika miradi ya Elimu na Afya huku akizungumzia ufadhili wa masomo ya kidato cha tano na sita na elimu ya juu kwa wanafunzi wanaofaulu vizuri na wanaotoka kwenye  mazingira magumu unaotolewa na Benki hiyo.

Walimu wakuu wa shule zilizopokea misaada hiyo wameishukuru Benki ya NMB kwa kuwapatia samani hizo ambazo zitasaidia kupunguza msongamano katika shule hizo ambazo zimekuwa na wanafunzi wengi huku wakiomba wadau wengine pia kuendelea kujitolea vifaa hitajika katika miundombinu ya elimu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita John Wanga akijibu changamoto za miundo mbinu ya kituo cha Afya katoro zilizotolewa na Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Dr. Rhoda Haule amesema kuwa kukamilika kwa Mradi wa Hospitali ya Wilaya katoro unaoendelea kwa sasa kutapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto zinazokikabili kituo hicho cha Afya na kuboresha huduma  kwa wananchi wote wa Katoro na maeneo jirani.

Aidha Mkurugenzi Wanga ametumia nafasi hiyo kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Bilioni 2.2 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo sambamba na kiasi cha shilingi milioni 600 zilizotolewa kwa ajili ya Mradi wa kupanga, kupima na kumilikisha Ardhi, fedha zilizotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Msaada huo uliotolewa na Benki ya NMB umezinufaisha Shule ya Sekondari Bahari na shule za Msingi Msufini, Mtakuja, Magenge,  Mchongomani, pamoja na kituo cha Afya Katoro.                              


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa