• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

"HAKUNA MCHANGO WOWOTE WA KUMZUIA MTOTO KWENDA SHULE" RC SHIGELA

Posted on: May 7th, 2023

Na. Michael Kashinde

Wito umetolewa kwa wananchi na viongozi wa kata ya Lwamgasa  kuhakikisha hakuna mtoto anayeshindwa kwenda shuleni kwa visingizio vyovyote ikiwemo michango mbalimbali, kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha miundombinu ya Elimu na kutoa Elimu bila malipo ili kumsaidia kila mwanafunzi apate Elimu bora katika mazingira bora bila kuathiriwa na changamoto kama hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa wito huo May 6, 2023 wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Lwamgasa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la zahanati ya Lwamgasa ambapo amesema kuwa michango yoyote ile isizuie mtoto kwenda shule na kama kuna utaratibu wa kuchangia chochote lazima kwanza ashirikishwe Mhe. Mkuu wa Wilaya.

RC Shigela ameendelea kusema kuwa dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona kila mtanzania anapata huduma bora za msingi ikiwemo Elimu na Afya na ndio maana kwa kuangalia hilo ametangaza ajira zaidi ya 12,000 katika Sekta hizo za Afya na Elimu ili kuongeza nguvu katika kuwahudumia watanzania, huku miundombinu ya umeme, maji na barabara ikiendelea kuboreshwa pia.

Amewasisitiza wananchi hao ambao wengi wao wanajihusisha na shughuli za uchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu kuwapeleka watoto wao shule ili wasome na kupata ujuzi wa kitaalamu ili miaka ijayo waweze kuwa wataalamu katika sekta mbalimbali na hata wakiendelea kufanya shughuli za uchimbaji basi wawe wachimbaji na wawekezaji wakubwa kwa maendeleo ya Taifa lao.

Ametoa rai pia ya kuwalinda watoto wa kike ili wasome na kufikia malengo yao badala ya kuwalaghai kimapenzi na kuwaharibia maisha huku akiwasisitiza kuwa na maelewano ya kimkataba kati ya mwenye ardhi na mwekezaji katika eneo husika kwa njia ya fidia au makubaliano mengine yanayoeleweka ili kila mmoja anufaike kwa nafasi yake, huku akiahidi kuwa Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuwarisishia njia mbalimbali za kufanya shughuli zao ikiwemo upatikanji wa leseni.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP. Safia Jongo ametoa rai kwa wananchi hao kutojichukulia sheria mikononi katika kutatua masuala mbalimbali badala yake wavishirikishe vyombo vya dola vyenye jukumu la kusimamia masuala ya kiusalama huku akisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wale wote wanaojihusisha kwa uvunjifu wa amani kupitia ushirikiana wakiwemo baadhi ya waganga wa kienyeji.

Katika kukomesha matukio ya kutoa na kupokea rushwa ACP. Safia amezungumza na wananchi wa Kata ya Lwamgasa akiwaambia kuwa huduma ya dhamana katika vituo vya Polisi ni bure hivyo mwananchi yeyote akiombwa fedha ya dhamana katika kituo cha Polisi asikubali huku akitoa namba zake za simu kwa wananchi hao ikiwa ni njia rahisi ya kuwasaidia kwa haraka endapo kuna matukio yoyote ya uvunjifu wa amani.

Akiwa katika ziara yake ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita  RC. Shigela alianzia katika kata ya Lwamgasa kwa kuzindua na kuweka jiwe la Msingi katika shule ya Sekondari Msisi zoezi lililoambatana upandaji miti katika viwanja vya shule hiyo, kabla ya kuelekea kuzindua kiwanda cha kuchakata Dhahabu cha Isra ziara iliyohitimishwa katika eneo la zahanati ya Lwamgasa kwa ukaguzi wa zahanati hiyo na mkutano wa hadhara sambamba na kujibu kero mbalimbali za wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuchakata Dhahabu cha Isra amesema kuwa Serikali inaendelea kuwasaidia wawekezaji kufanya kazi katika mazingira salama na wezeshi ili kulinda mitaji yao huku akiendelea kuhamasisha ushirikiano kati ya wananchi na wawekezaji ili kuendelea kutengeneza fursa za ajira kwa maendelea ya wananchi wa maeneo husika na taifa kwa ujumla.



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa