• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

GEITA DC YAJIPANGA KUKABILIANA NA MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI

Posted on: May 31st, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imejiwekea mikakati mahususi ya kukabiliana na matumizi holela ya mifuko ya plastiki, ikianza na maeneo ya soko la CCM Katoro, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Mazingira Duniani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki hiyo Mei 31, 2025, katika viwanja vya CCM Katoro, Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira katika halmashauri hiyo, Bw. David O. Mlahagwa, amesema kuwa hatua madhubuti zitachukuliwa kwa watakaobainika kutumia mifuko hiyo kinyume cha sheria.

“Mkakati wetu wa kwanza ni kufanya ukaguzi katika maduka yote. Tukikuta mtu anatumia mifuko ya plastiki, tutamchukulia hatua za kisheria. Pili, tutadhibiti aina ya mifuko inayotumika kama vifungashio ambayo huruhusiwa, lakini haitakiwi kurudi kwa wananchi baada ya matumizi,” amesema Mlahagwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ndg. Karia Magaro, amewataka wafanyabiashara wa soko la Katoro kuendeleza jitihada za usafi katika maeneo yao.

“Niendelee kuwaomba tuhamasishane, na kila mmoja ahakikishe eneo lake linafanyiwa usafi,” amesisitiza Magaro.

Akihitimisha, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, ametoa rai kwa wananchi kutokutupa ovyo bidhaa za plastiki na kuacha kabisa matumizi ya mifuko hiyo.

“Tusitupe chupa wala mifuko ya plastiki hovyo. Plastiki haitooza; itatuharibia mazingira yetu, na baadaye mazingira hayo yatatuathiri sisi wenyewe,” amesema Komba.


Uzinduzi huo ulitanguliwa na zoezi la usafi katika maeneo ya soko hilo, likishirikisha watumishi wa halmashauri, wafanyabiashara na wakazi wa eneo hilo.

Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Juni, kufuatia uamuzi wa mwaka 1972 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP), linalolenga kuhamasisha ulinzi wa mazingira duniani kote.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI ASISITIZA HATUA KUCHUKULIWA KUDHIBITI UTORO SHULENI.

    June 05, 2025
  • MKURUGENZI ASHIRIKI BONANZA LA WATUMISHI GEITA.

    May 17, 2025
  • MSUKUMO WATOLEWA UKAMILISHAJI WA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 763.6 GEITA DC

    June 05, 2025
  • MKOA WA GEITA KUELEKEA IRINGA KUSHIRIKI UMITASHUMTA.

    June 03, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa