• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

ELIMU YA AFYA KUWA AJENDA YA KUDUMU KATIKA VIKAO VYA MAENDELEO YA KATA NA VIJIJI GEITA DC

Posted on: April 15th, 2023

Na Michael Kashinde

Kamati ya uelimishaji, uhamasishaji na ushirikishwaji wa jamii kuhusu kujikinga na magojwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika kikao chake cha Aprili 14, 2023 imeazimia kulifanya suala la Elimu ya Afya kwa Umma, kuwa ajenda ya kudumu katika vikao vya maendeleo ya kata na vijiji ili kuwajengea wananchi uelewa wa namna ya kujikinga na magonjwa mbalimbali yakiwemo ya milipuko.

Kamati hiyo inayoundwa na jumla ya wajumbe 45 kwa ngazi ya Halmashauri ambao ni wataalamu na viongozi mbalimbali katika jamii inaamini kuwa kutekelezwa kwa azimio hilo kikamilifu kutaisaidia jamii kupata Elimu ya kujikinga na magonjwa mbalimbali yakiwemo ya milipuko ambayo wakati mwingine yanaweza kusababishwa na uzembe au uelewa mdogo wa baadhi ya watu katika Jamii.

Bw. Ezrael Tarimo Afisa mifugo Halmashauri ya Wilaya ya Geita akitoa ufafanuzi wa namna idara ya Kilimo pamoja na mifugo zinavyoshiriki katika kuikinga jamii na magonjwa ambayo wakati mwingine husababishwa na hali za afya za wanyama hao au matumizi ya dawa muda mfupi kabla ya kuchinjwa, amefafanua kuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuna utaratibu mzuri wa kukagua wanyama na kujiridhisha kabla ya kutoa vibali vya kuwachinja unaosimamiwa na wataalamu wa mifugo kwa lengo la kudhibiti hali hizo.

Bw. Tarimo ameendelea kusema kuwa utaratibu huo hautofautiani na unaotumika katika idara ya kilimo huku akitoa rai kwa jamii kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa idara hizo katika jamii zao pale wanapoona baadhi ya wakulima au wafugaji wanakiuka taratibu hizo ikiwemo kupulizia dawa muda mfupi na kupeleka mazao sokoni ili kuikinga jamii kuathirika na madhara kama hayo.   

kwa upande wake Afisa uelimishaji, uhamasishaji na ushirikishwaji jamii kutoka Wizara ya Afya sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma Bi. Magdalena Dinawi, akieleza majukumu ya kila mjumbe katika kamati hiyo katika ukumbi wa Hospitali ya Wilaya Nzera, amemtaka kila mjumbe kwa nafasi yake kuwajibika kikamilifu kwa kufikisha Elimu sahihi kwa jamii ili kuongeza uelewa zaidi kuhusu kujikinga na magonjwa.

Aidha Bi. Dinawi amewataka wajumbe wa kamati hiyo kuanza kutekeleza majukumu yao kuanzia sasa kwa kuandaa mipango kazi, kutoa misaada ya kitaalamu kwa wajumbe na jamii kwa ujumla ili kujenga uwezo wa kufanya usimamizi wa kazi zote za Kamati hiyo sambamba na kuisaidia jamii na kuiwezesha kushiriki shughuli mbalimbali yakiwemo majanga na dharura.

Naye mratibu wa kamati hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi. Frida Mkwama akizungumza wakati wa kikao hicho amesisitiza kuwa Elimu ya Afya ni tiba nzuri, huku akitoa wito kwa wajumbe hao wakiwemo viongozi wa dini ambao jamii inawaamini kwa kiasi kikubwa, kutumia majukwaa yao na nyumba za ibada kutoa Elimu hiyo ya Afya kwa jamii ili Elimu hiyo iwafikie wananchi wote na kwa njia rahisi.

Kamati hii ina jukumu kubwa la kuielimisha jamii, kuihamasisha na kuishirikisha kuhusu kujikinga na magonjwa mbalimbali hasa katika nyakati hizi ambazo karibia kila kukicha hapa duniani yanaibuka magonjwa ya milipuko, hivyo basi jukumu hili halibaki tu kwa kamati bali kila mmoja kwa nafasi yake anawajibika kujikinga na kuwakinga wengine pia kwa kufuata taratibu mbalimbali zinazoshauriwa na wataalamu ili kujiweka katika mazingira salama kwa kuwa hata mimi binafsi naamini kuwa Afya bora ni Msingi wa maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla hivyo tunawajibika kulinda Afya zetu..



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa