• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DKT SAMIA AMEILINDA HESHIMA YA KIONGOZI ALIYEMTANGULIA

Posted on: August 13th, 2024

Katoro-Geita

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi amesema Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelinda heshima ya kiongozi aliyemtangulia kwa kuendeleza miradi mikubwa afrika Mashariki.

Mamia ya wananchi wakiwa katika viwanja vya CCM-Katoro wakifuatilia Mkutano wa Hadhara wa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM), Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi

Akizungumza na wananchi kata ya Katoro halmashauri ya wilaya ya Geita wakati wa ziara yake Agosti 12, 2024, Balozi Dkt Nchimbi  ameitaja miradi mikubwa Mhe Dkt Samia ameiendeleza ni pamoja na mradi wa treni ya umeme kutokea Dar es Salaam kwenda Mwanza ambayo Hayati Magufuli alianza kuijenga na hadi kifo chake mradi huo ulikuwa umefika KM 722 na kusema Mhe Dkt Samia katika awamu yake ameweza kujenga km 1506 na kwa upande wa mradi wa bwawa la umeme ambao ulikuwa umefika asilimia 36 ambazo ziliachwa na mtangulizi wake na kwa sasa mradi huo umefika asilimia 98.4. “Amelinda heshima ya kiongozi aliyemtangulia” amesema Balozi Dkt Nchimbi.

Mhe Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela akizungumza katika Mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM, Uliofanyika Kata ya Katoro ambapo, Balozi Dkt Nchimbi amepongeza uongozi mzuri wa Mkuu huyo wa Mkoa katika kusimamia shughuli za kiserikali ndani ya Mkoa wa Geita.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Busanda wilaya ya Geita Mhandisi Tumaini Magesa amemuomba katibu Mkuu wa chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi, kuendelea kushughulikia suala la hitaji la kuwa na Halmashauri kwa wananchi wa jimbo la Busanda kwakuwa kumekuwa na idadi kubwa ya wananchi

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM) Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi  amehutubia mamia ya wananachi katika viwanja vya CCM-Katoro ambapo amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amelinda heshima ya kiongozi aliyemtangulia kwa kuendeleza miradi mikubwa ikiwepo ya ujenzi wa Reli ya kisasa

Naye Naibu Waziri wa mambo ya ndani Daniel Bassil Sillo amesema kuwa serikali imeanza mchakato wa kuupandisha hadhi ya mji mdogo wa katoro kuwa wilaya ya Kipolisi ili kuendelea kuboresha huduma za usalama katika mji huo kutokana na kuwa naongezeko kubwa la watu. Sillo amesema amepokea changamoto hiyo kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Busanda Mhandisi Magesa juu ya ombi la mji huo kuwa Halmashauri.

Pamoja na hayo ziara ya Mhe Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi imelenga kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia majibu ambapo jumla kero 108 kutoka kwa wananchi 61 zilipokelewa na kutoa ufumbuzi wa kero hizo, huku baadhi zikikabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela kuzishughulikia.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa