• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DED GEITA AFANYA ZIARA KATIKA MRADI WA JENGO LA UTAWALA LA GEITA DC

Posted on: September 26th, 2023

Na: Hendrick Msangi NZERA.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndugu Karia Rajabu Magaro, amefanya ziara kwenye jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Mhandisi Shilingo akimuonyesha ramani ya Jengo la Halmashauri kwa Mkurugenzi ndugu Karia Rajabu Magaro alipotembelea jengo hilo kukagua hatua za ujenzi wake.

 Katika Ziara yake yenye lengo la kukagua hatua za ujenzi wa Jengo hilo. 

Magaro aliambatana na Wakuu wa Idara mbalimbali za Halmashauri ili waweze kuona kazi inavyoendelea na pia kushauri hatua za kuchukua kuelekea kukamilika kwa jengo hilo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndugu Karia Rajabu Magaro akizungumza na wakuu wa Idara mbalimbali Kwenye Halmashauri hiyo alipotembelea kukagua ujenzi wa Jengo hilo ambalo watumishi wa Halmashauri watahamia Mwezi Octoba.

Katika ziara hiyo Mkurugenzi Magaro alimtaka Mhandisi Shilingo ambaye ni Kaimu Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuhakikisha anafuatilia mafundi kuwepo site muda wote ili kukimbizana na kazi iliyobaki, pamoja na kuhakikisha vifaa vyote yakiwemo materials ambayo hayajatumika yanahifadhiwa sehemu salama pamoja na  kuwa Documented kutunza  kumbukumbu.


Aidha alimtaka Mhandisi Shilingo kufanya kazi kwa kasi huku ramani ya jengo hilo ikizingatiwa. 


‘’ Unatakiwa uwe Site Engeneer badala ya kukaa  ofisini ili kuja kujionea kazi ambazo mafundi wanazifanya na kutoa ushauri wa kitaalam’’ alisema Magaro.

Pamoja na hayo Mkurugenzi huyo ilipendekeza kuwe na kamati maalum kwa ajili ya kuratibu kazi zote zilizobaki ili kufikia lengo la kuhamia katika jengo hilo.


 ‘’Kuwe na kamati yenye mpango mkakati na ije na mrejesho wa hatua zilizochukuliwa kukamilisha kazi hii ili tunaposema tunaingia mwezi wa kumi tufikie hilo lengo na iwapo kuna changamoto basi nielezwe’’; alisema Magaro kwa watumishi hao.


Ujenzi wa Jengo hilo ulio anza tarehe 22 mwezi Februari  mwaka 2022 unakaribia kukamilika mapema mwezi ujao , na watumishi kuingia rasmi ifikapo Octoba 15, mwaka huu.


Gharama za Ujenzi zilizotumika mpaka sasa ni kiasi cha shilingi Bilioni mbili na laki saba ambazo zimejumuisha ujenzi wa jengo la utawala, uzio, majengo ya kibenki, kibanda cha mlinzi na kibanda cha nishati ya umemeKwa mujibu wa Mhandisi Shilingo , Ujenzi wa Jengo hilo umekamilika kwa Asilimia 95 mpaka sasa. 


Ujenzi huo  ni sehemu ya miradi inayotekelezwa na  Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo Serikali kuu inayo ongozwa na Mh Dkt Samia Suluhu Hassan , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaelekeza fedha nyingi kwenye miradi ili kuwaletea wanachi huduma bora na maendeleo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa