• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO AWATAHADHARISHA WAKULIMA KUUZA MAZAO YA CHAKULA KWA KIASI NA KUBAKIZA ZIADA

Posted on: September 7th, 2022

Na Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo amewataka viongozi na watumishi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuwahamasisha wananchi kufanya kilimo cha kisasa ili kuongeza uzalishaji huku akisisitiza kuwa na tahadhari katika kuuza mazao hayo ya chakula ili kubaki na ziada ya kutosha katika matumizi ya chakula katika ngazi za familia.

Mhe. Shimo ameyasema hayo Septemba 6, 2022 akiwa  katika siku ya kwanza ya  mkutano wa nne wa kawaida wa baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2021/2022 uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera ambapo mkutano huo umepokea na kupitisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa kipindi cha Mwezi Aprili hadi Juni 2022.

Mhe. Shimo amesema kuwa ni vyema wananchi wakahamasishwa kufanya kilimo cha biashara huku akieleza kuwa kuna mchakato maalumu wa kilimo unaoandaliwa ambapo kila Kata itahamasishwa na kuwa na zao lake kuu litakalolimwa katika eneo husika suala litakalosaidia katika kuongeza ubora, uzalishaji, kuitangaza kata husika pamoja na kurahisisha masoko ya mazao hayo.

Aidha DC Shimo ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa viongozi na watumishi mbalimbali kuwakumbusha wananchi kuuza vyakula kwa kiasi ili wabaki na ziada ya chakula katika familia zao, kwa kuwa mamlaka za hali ya hewa zimetoa taarifa ya uhaba wa mvua kwa mwaka huu hali inayoleta hofu ya njaa ingawa mpaka sasa bado Wilaya ya Geita ina chakula cha kutosha.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu ameshukuru kwa kusema kuwa baraza lake limepokea ushauri uliotolewa na viongozi mbalimbali wa Wilaya na kusisitiza kuwa ni jukumu la madiwani kuwahamasisha wananchi kufuata maelekezo ya viongozi mbalimbali Serikali kwa kutumia vikao vyao vya maendeleo ya Kata.

Mhe. Kazungu ameendelea kwa kusema kuwa suala la kilimo cha aina moja katika kila Kata ni suala jema ambalo litasaidia Kata hizo kutambulika kwa uzalishaji wa mazao husika yatakayokuwa yakilimwa katika maeneo hayo.  

Wakati huo huo  Madiwani mbalimbali wakiwasilisha taarifa za utekelezaji wa maendeleo katika Kata zao kuhusu Sekta ya kilimo wamesema kuwa wananchi wamehamasika kulima mazao mbalimbali ya chakula na biashara kama vile Mahindi, Maharage, Pamba, viazi vitamu, mihogo, ndizi, na mengine mengi.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo katika Kata ya Isulwabutundwe iliyowasilishwa na diwani wa Kata hiyo Mhe. Maweda Gwesandili amesema kuwa wakulima waliolima mazao ya biashara na chakula tayari wameanza kuvuna ambapo kwa sasa bei ya mahindi ni Tshs. 68,000/= huku mpunga ukiwa ni Tshs. 90,000/= kwa gunia.

Kwa upande wa mazao ya biashara taarifaya Kata hiyo imeeleza kuwa wananchi wengi walihamasika kulima zao la pamba ambapo mpaka sasa wamefanikiwa kuvuna pamba hiyo kiasi cha Kg 29,819 na kuipeleka katika maghala ambapo wamekuwa wakiuza kwa bei ya kati ya Tshs. 1800 na Tshs. 1900 kwa kilo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa