• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO AWALAZA NDANI MAFUNDI NA WASIMAMIZI WA MIRADI YA TASAF (CMC) KWA KUTOTIMIZA WAJIBU WAO KIKAMILIFU

Posted on: August 3rd, 2022

Na Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe.Wilson Shimo akiwa na kamati ya ulinzi na usalama Wilaya, katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya  Geita Agosti 3, 2022 amewaweka ndani Mafundi na wasimamizi wa miradi ya TASAF baada ya kuonekana dosari zilizosababishwa na uzembe wao katika Miradi wanayoisimamia huku akiwataka wahusika hao kurekebisha haraka dosari hizo mara tu atakapowatoa.Waliokutana na adhabu hiyo ya Mhe. Shimo ni Bw.Stephen Kayogo ambaye ni fundi Mkuu Shule ya Msingi Makatani  katika kijiji cha Ihumilo, Bw. Mathayo Mgongo ambaye pia ni fundi Mkuu katika Mradi wa Nyumba ya Mtumishi katika shule ya Msingi Nyamikoma kijiji cha Lwenge, Bw.Emmanuel Masondole ambaye ni Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Lwenge na Bw. Juma Richard ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya ujenzi katika mradi huo.

 Mhe. Shimo akiwa na Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya, ameanza ziara yake kwa kutembelea mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ofisi moja ya Mwalimu pamoja na matundu sita ya vyoo, uliotengewa kiasi cha Tshs.66,845,000/= ambapo nguvu za wananchi katika mradi huo ni Tshs.7,899,000/=   ambapo kwa sasa mradi uko katika hatua ya kupauliwa kwa upande wa vyumba vya madarasa na ofisi ya Mwalimu.Baada ya kupokea taarifa na kukagua mradi huo Mhe. Shimo ametoa wiki mbili kwa wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanawasiliana na Mzabuni wa vifaa ili avilete haraka na kazi iendelee huku akiitaka kamati ya ujenzi wa mradi huo kufuatilia kila hatua ya mradi na kurekebisha haraka dosari zilizojitokeza sambamba na kuwahamasisha wananchi kuchangia nguvu zao katika mradi huo ili shule zitakapofunguliwa uwe tayari kutumika.

DC Shimo ametembelea mradi wa ujenzi wa nyumba ya watumishi ya Two in One katika Zahanati ya Shilamena mradi uliofikia katika hatua ya kuelekea kupaua ambapo amewapongeza wasimamizi wa mradi huo kwa umakini na ubora unaoonekana katika mradi huo huku akitoa ushauri wa kuvuta umeme katika zahanati hiyo ambayo hivi karibuni itaanza kutoa huduma ili kuboresha na kurahisisha huduma  mbalimbali hasa za uzazi.

Katika kijiji cha Lwenge kuna mradi wa mpango wa TASAF ambao ni ujenzi wa nyumba ya Mwalimu Two in One katika shule ya Msingi Nyamikoma ambao TASAF makao makuu wametoa kiasi cha 100,045,892 ikiwa ni  90% ya mradi husika huku nguvu za wananchi zikiwa ni 10% ili kuukamilisha.

Viongozi wa Mradi huo akiwemo fundi mkuu wametakiwa kurekebisha haraka dosari zilizobainishwa na Kamati hiyo ya ulinzi na usalama Wilaya sambamba na kuendelea kuhamasisha wananchi kutumia nguvu zao ili kuongeza kasi ya mradi huo.

Mathayo Kuzenza na Daniel Selemani wameishukuru Serikali chini ya Rais Samia kwa kuwaletea miradi hiyo ambayo imekuwa na tija kwa wananchi hao akitolea mfano wa kipindi cha nyuma wao walikwenda umbali mrefu kwa ajili ya kupata Elimu ingawa kipindi cha masika walishindwa kwenda kwa kuwa kulikuwa na mto uliokuwa unajaa na kuziba njia ambapo kwa sasa kwenye eneo lile la mto pamejengwa daraja na Shule imesogezwa katika kijiji chao.Akifunga siku ya kwanza ya ziara yake katika miradi ya TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Shimo amewataka wale wote waliopewa nafasi ya kusimamia na kujenga miradi hiyo kushiriki kikamilifu katika kutimiza wajibu huo ili miradi hiyo iwe na ubora unaotakiwa huku akisisitiza kuwa hatua anazozichukua dhidi ya wanaozembea ni katika kuwakumbusha kutekeleza wajibu wao kwa maslahi ya Taifa huku akimshukuru Rais Samia kwa kuipatia Wilaya ya Geita miradi mingi na yenye tija kwa wananchi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa