• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO ATAJA MIGOGORO YA KIFAMILIA KUWA CHANZO CHA UKATILI KWENYE JAMII

Posted on: November 29th, 2022

Na. Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo ametoa rai kwa wanawake na watoto katika jamii kuepuka migogoro katika familia ambayo inaweza kuchangia kufanyika kwa vitendo vya ukatili.

Amezungumza hayo Novemba 29, 2022 katika ukumbi wa JJ Katoro wakati akifungua maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita maadhimisho yaliyoanza Novemba 25 na kutarajiwa kuhitimishwa Disemba 10, 2022.

DC Shimo amesema kuwa hata wanawake wanapaswa kuacha ukatili kwa wanaume huku akitolea mfano baadhi ya lugha kali zinazotumiwa na wanawake dhidi ya waume zao  ambazo wakati mwingine zinakuwa chanzo cha migogoro inayopelekea vitendo vya ukatili.

Wakati huo huo amewataka watoto pia katika familia kuacha chokochoko  ambazo zinaweza kuwapunguzia uwajibikaji wakakosa heshima na adabu suala linaloweza kuchangia wazazi au walezi kutoa adhabu au vipigo vinavyotokana na hasira suala ambalo ni ukatili pia.

Aidha DC Shimo ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kushirikiana na wadau wa kupinga ukatili kwa kuendeleza juhudi za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kamati za kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto  katika kata zote 37 za Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akitoa neno la shukrani kwa Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Adv. John Wanga amesema Halmashauri ya Wilaya ya Geita imepokea maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na mgeni rasmi huku akiahidi kushirikiana na wadau mbalimbali kuyasimamia mabaraza ya watoto ya kupinga ukatili ili yawe chachu ya kupeleka taarifa hizo katika jamii zetu.

Adv. Wanga ameendelea kwa kusema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kutoa mikopo ya asilimia 10 kwa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ikiwa ni fursa ya kuwajengea uwezo wa kujitegemea ili wasiwe dhaifu kiuchumi.

Awali akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi. Enedy Mwanakatwe amesema kuwa kesi za ukatili ambazo zimekuwa zikipokelewa kutoka katika makundi mbalimbali ya kinamama na watoto ni pamoja na ukatili wa kisaikolojia, kimwili, kingono na kiuchumi ambapo kwa kipindi cha Mwezi Januari hadi Oktoba 2022 matukio yaliyotolewa taarifa ni 26 ambapo ubakaji ni matukio 7, ulawiti ni  2 na vipigo ni 17.

Bi. Mwanakatwe ameendelea kusema kuwa pamoja na matukio hayo kutolewa taarifa na wanawake na watoto lakini pia baadhi ya wanaume wamekuwa wahanga wa ukatili japokuwa hawatoi taarifa katika Ofisi hizo za maendeleo ya jamii suala ambalo linatia ugumu kupata taarifa zao sahihi.

Aidha Bi. Mwanakatwe amesema kuwa katika kutekeleza mpango kazi wa Taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto Halmashauri imefanikiwa kuunda mabaraza ya watoto na kamati za MTAKUWA ili kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto huku akiwashukuru wadau wanaoshirikiana na halmashauri kufanikisha juhudi hizo.

Maadhimisho hayo yameanza na maandamano ya hiyari katika Kata ya Katoro yakiwashirikisha wananchi na wadau mbalimbali waliokuwa na mabango ya jumbe za kupinga ukatili ambapo pia elimu ya Kupinga ukatili imetolewa kwa wananchi waliojitokeza.

Miongoni mwa mashirika ambayo ni wadau wakubwa wa kupinga ukatili wanaofanya kazi na Halmashauri ya Wilaya ya Geita ni pamoja na PLAN International, VSO, PATWAO, Dawati la jinsia kutoka jeshi la Polisi, SEDIT, Marafiki wa elimu,Bright Light, Gelao na SMAUJATA. 

 

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa