• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO APONGEZA UANZISHWAJI WA SHULE MPYA GEITA DC BADALA YA KUONGEZA MADARASA

Posted on: October 29th, 2022

Na. Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Samwel Shimo ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa mpango wake wa kuanzisha shule mpya za sekondari badala ya kuongeza majengo ya vyumba vya madarasa katika shule zilizopo hali inayofanya kuwa na majengo mengi katika shule moja.

DC Shimo ametoa pongezi hizo Oktoba 28, 2022 akiwa katika mkutano wa kawaida wa  baraza la madiwani kwa robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2022/2023 uliofanyika Oktoba 27 na 28 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Nzera.

Ameendelea kusema kuwa kuanzishwa kwa shule mpya hizo kunapunguza changamoto ya shule moja kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi kuliko kawaida lakini pia ni msaada mkubwa kwa wanafunzi kwa kuwa hawataathirika na umbali kutoka nyumbani kwenda shuleni kila siku.

Wakati huo huo Mhe. Shimo ametoa rai kwa Halmashauri na madiwani kuhakikisha wanafuatilia kwa karibu mabaraza ya kazi, utendaji wa viongozi wake  na namna yanavyofanya kazi kwa ujumla sambamba na kuyasaidia pale yanapohitaji msaada zaidi, huku akiwakumbusha pia kutoa taarifa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya pale wasikiapo malalamiko ya rushwa kutoka kwa wananchi katika shughuli za utendaji wa Mahakama za mwanzo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Barnabas Mapande baada ya kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa fedha za ujenzi wa madarasa ya shule za sekondari, ametoa wito wa kusimamia vizuri ujenzi wa vyumba hivyo 267 vinavyojengwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita na kuvikamilisha kwa wakati huku akisisitiza kuwa, kwa kufanya hivyo ni kumuunga mkono Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan aliyeguswa kuwasaidia watoto wengi wa hali ya chini kwa kuwajengea miundombinu bora na ya kisasa.

Aidha ametumia nafasi hiyo kuwaomba viongozi mbalimbai watakaotakiwa kutoa ushirikiano katika kufuatilia malipo ya watumishi waliotolewa kazini kwa mchakato wa vyeti feki kufanya hivyo, ili kuwasaidia watumishi hao kupata haki yao, huku akiendelea kuzitaka mamlaka husika kuzuia wananchi mapema wanapotaka kuanza kulima katika maeneo yaliyozuiwa na Serikali badala ya kuchelewa na kuja kufyeka tayari yakiwa chakula.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu ametoa wito kwa madiwani kushirikiana na watendaji wa maeneo yao katika kusimamia vizuri miradi ya mendeleo ambayo inaendelea kujengwa katika kata zao kwa kuzingatia ubora unaotakiwa kuanzia kwenye ununuzi wa matofali na vifaa vingine vinavyotumika katika ujenzi.

Aidha amesisitiza kuwa Halmashauri imepokea ushauri uliotolewa na wajumbe na viongozi mbalimbali kuhusu mambo yote yaliyojadiliwa kwa siku mbili za mkutano huo, huku akiwataka  madiwani kuona umuhimu wa kupata gari la zimamoto kwa ajili ya kudhibiti ajali za moto hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali inajenga miradi mikubwa na yenye kutumia fedha nyingi kwa kuwa mpaka sasa Halmashauri haina gari la zimamoto. 

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Adv. John Wanga akijibu hoja mbalimbali zilizojadiliwa katika mkutano huo amesema kuwa katika kudhibiti suala la ujenzi holela Timu ya Menejimenti inaandaa andiko kwa ajili ya kuweka utaratibu wa matumizi bora ya ardhi ili kudhibiti ujenzi holela katika maeneo yanayokua kwa kasi.

Aidha Adv. Wanga amefafanua kuwa Timu ya Menejimenti imebaini kuwa ujenzi huu holela unasababishwa na uuzwaji wa ardhi kiholela katika maeneo yanayokua kwa kasi kutokana na uwepo wa huduma ya umeme wa REA  ambapo Halmashauri imeamua kuja na mkakati wa kuunda kamati ndogondogo za usimamizi wa ardhi ambazo zitahakikisha mwananchi anayepata eneo kwa sasa anajenga bila kukosea.

Uwepo wa nishati ya umeme kwenye maeneo ya vijijini kupitia mpango wa REA umeleta mabadiliko makubwa katika maeneo hayo kwa kuwa yamekuwa yakikua kwa kasi na kukua kwa huduma mbalimbali za kijamii suala ambalo linawavutia pia watu wengi kuwekeza katika maeneo hayo ambapo kwa kuliona hilo Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeona kuna haja ya kuchukua hatua mapema.

Katika mkutano wa siku mbili wa robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2022/2023 baraza la madiwani limekamilisha shughuli mbalimbali ikiwemo kupokea na kupitisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo  kuanzia ngazi za kata, taasisi na Idara mbalimbali, sambamba na taarifa za kamati mbalimbali za kudumu, huku pia  maswali mbalimbali ya waheshimiwa madiwani yakitolewa  majibu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • UBORESHAJIWA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025 WAFIKIA KIKOMO GEITA.

    May 08, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa