• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO AKABIDHI MKOPO WA PIKIPIKI 5 ULIOTOLEWA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA KWA MAWEMERU BODABODA GROUP

Posted on: August 4th, 2022

Na Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe.Wilson Shimo Agosti 4, 2022 amekabidhi pikipiki tano (5) kwa kikundi cha Mawemeru bodaboda group kilichopo katika kata ya Nyarugusu ukiwa ni mkopo uliotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuwasaidia vijana kujikomboa kiuchumi.

Mkopo huo una thamani ya shilingi 15,000,000/= ambapo umehusisha ununuzi wa pikipiki 5 kwa thamani ya shilingi 12,500,000/=  huku kiasi cha shilingi 2,500,000/= kikitumika kwa ajili ya kununua vifaa vya kujikinga baridi na kingine kilichobaki kikitumika kama mtaji wa kuanzia.Mhe.Shimo akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama Wilaya sambamba na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita amewapongeza vijana hao kwa ujasiri wa kufuata taratibu zote za kupata mkopo huo huku akitoa wito kwa waendesha bodaboda wote kufuata taratibu zote za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanakuwa na Leseni na bima huku akiwakumbusha kutopuuzia kufunga vifaa ya kuzimia moto katika vyombo yao kama alivyoeleza awali Insp. Edward Lukuba Afisa Zimamoto Wilaya ya Geita akizungumza na madereva hao.Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Adv. John Wanga amesema kuwa kikundi hicho kilipitiwa na Mwenge wa Uhuru Julai 21 mwaka huu ambapo kiongozi wa mbio za Mwenge aliagiza kukata bima kubwa na leseni kwa kila dereva suala ambalo tayari limekamilishwa 100%.

Aidha Adv.Wanga ametumia pia nafasi hiyo kualika makundi mbalimbali wakiwemo vijana, wanawake na makundi maalumu kufuatilia utaratibu wa kupata mikopo isiyo na riba katika Halmashauri  huku akisisitiza fedha hizo zipo kwa ajili yao ili kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake Afisa vijana Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bw. Alex Herman akizungumzia mkopo huo amesema kuwa ana matumaini ya kuona mafanikio kwa kikundi hicho kwa kuwa takwimu zinaonesha 90% ya vikundi vinayochukua mikopo ya bodaboda vimekuwa vikifanikiwa  vizuri kwa kuwa vijana wa bodaboda hawana usumbufu katika marejesho.

Akizungumzia mkopo huo Bw.Leonard Nkalango ambaye ni mwanachama kikundi wa Mawemeru Group ameishukuru Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kuwapatia mkopo huo bila riba pamoja na ushauri wa kitaalamu kuhusu upanuzi na usimamizi wa miradi ambapo pia ameeleza kuwa wamejipangia utaratibu kwa kukusanya kiasi cha shilingi 10,000/= kila siku kwa kila mmoja na kuweka kwenye Akaunti yao kwa ajili ya marejesho.Mawemeru bodaboda group ni kikundi kilichoanza rasmi mnamo mwaka 2021 kikiwa na mtaji wa shilingi 200,000/= tu ambazo walizitumia kukopeshana ili kujikwamua kiuchumi kabla ya kupatiwa mkopo wa shilingi 15,000,000/= ambapo rejesho lao la kwanza linatarajiwa kuwa Septemba 29 mwaka huu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa