• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO AITAKA JAMII KUWEKA ULINZI KWA WATOTO ILI KUDHIBITI UKATILI KWA WATOTO

Posted on: June 16th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo akiwa katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika ki Wilaya katika shule ya sekondari Lwezera Halmashauri ya Wilaya ya Geita Juni 16, 2022 amekemea ukatili mbalimbali unaofanywa na jamii kwa kujua ama kutokujua.

Mhe. Shimo ametumia maadhimisho hayo kuainisha vitendo mbalimbali vya kikatili wanavyofanyiwa watoto kwenye jamii zetu, huku akikemea vitendo hivyo na kuitaka jamii kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto ndani ya familia ili kuwalinda na mazingira mbalimbali hatarishi.

Miongoni mwa vitendo vya ukatili kwa Watoto alivyovikemea Mhe. Shimo ni pamoja na kutowapeleka shule na kufuatilia maendeleo yao, kuwapiga na kutoa adhabu kali, huku akisisitiza suala la kukaa shuleni muda mrefu bila kula ni ukatili pia na kuitaka jamii kuchukua hatua.

Aidha amemtaka kila mtu katika jamii kuhakikisha anatimiza wajibu wake kwa kuhusika kuwalea kimaadili watoto katika familia zao kuliko kuwaacha wakachangamana na watu wengine ambao wanaweza kuwa sio wema na kuwafunza mambo yasiyofaa katika jamii.

Mhe. Shimo ametumia nafasi hiyo Kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha kuwajali watoto na kuondoa ada kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita huku, huku akiendelea kuwahamasisha wananchi kushiriki katika zoezi la Sensa ya watu na makazi Agosti 23 na kutoficha taarifa zozote watakazoulizwa na makarani wa Sensa.

Naye Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Diwani wa kata ya Nyamigota Bi.Khadija Said Joseph akizungumza katika maadhimisho hayo amewataka wananchi waliojitokeza hapo kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao kwa kuwafikishia ujumbe wa siku ya Mtoto wa Afrika  unaolenga kupinga ukatili na kuhamasika kushiriki katika zoezi la Sensa.

Awali Akisoma risala kwa Mgeni rasmi Anjelina Phinias Mwanafunzi wa Darasa la Sita katika Shule ya Msingi Lwezera ametaja changamoto mbalimbali wanazokutana nazo watoto ikiwemo ukatili wa aina mbalimbali ambao mara nyingine huanzia ngazi za familia kwa kukosa pia usimamizi mzuri wa wazazi.

Kwa upande wake Afisa Lishe Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi. Tibezuka Mapesa ametumia nafasi hiyo kuwahamasisha wananchi kuzingatia lishe bora hasa kuanzia ngazi za familia  ili kuwasaidia watoto kukua vizuri kimwili na kiakili hali itakayosaidia kuepuka utapiamlo.

Maadhimisho hayo yameenda sambamba na burudani zenye jumbe mbalimbali kutoka katika vikundi mbalimbali ya watoto ambapo pia kulikuwa na zawadi kwa vikundi hivyo sanjari na kutoa misaada kwa watoto wenye uhitaji maalumu.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa