• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC SHIMO AHIMIZA KUIMARISHA ULINZI SHIRIKISHI ILI KUDHIBITI UHALIFU

Posted on: October 8th, 2022

Na. Michael Kashinde

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo akizungumza na wajumbe wa baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Oktoba 7, 2022 ametoa wito wa kuimarisha ulinzi shirikishi katika maeneo yote ya Wilaya ya Geita ili kudhibiti vitendo vya wizi.

Mhe. Shimo akizungumza na wajumbe hao katika mkutano maalumu wa baraza la madiwani  ulioketi katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Nzera, kupokea taarifa ya fedha kiasi cha Bilioni 5 na milioni 340 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 267 vya madarasa ya Sekondari, amesema kuwa licha ya kuimarisha ulinzi shirikishi ni vyema pia kuibua fursa za ujenzi wa vituo vya polisi kwenye maeneo yenye uhitaji wa haraka akitolea mfano wa eneo la Bukoli.

Aidha ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa namna inavyoendelea kufanya kazi zake huku akishauri kuongeza wigo wa kupata wazabuni kwa kanda, ili kuongeza ufanisi zaidi ya mwaka jana katika ujenzi wa madarasa ya UVIKO 19 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilifanikiwa kukamilisha kwa ubora unaotakiwa jumla ya vyumba 354 vya madarasa.

Awali Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Adv. John Wanga akijibu hoja mbalimbali za wajumbe hao katika Mkutano huo amesema kuwa Halmashauri imeunda kamati mbalimbali za usimamizi kwa lengo la kufanikisha kufanya kazi nzuri huku akitoa wito wa kushirikiana badala ya kusuguana.

Adv. Wanga amesema kuwa wamejipanga kwa kuwatumia wazabuni wenye uwezo wa kuifanya kazi hiyo kwa wakati sahihi, huku akieleza kuwahusisha wataalamu  katika kukagua ubora wa vifaa mbalimbali vitakavyotumika, wakiwemo TFS ambao watashiriki kukagua mbao zilizokomaa na zinazofaa kutumika.

Aidha ametoa wito kwa Madiwani hao ambao ndio wenyeviti wa WDC katika kata zao, kutoa taarifa kwa viongozi wa Halmashauri akiwemo yeye mwenyewe, pale wanapohitaji kuuliza kitu au kukutana na changamoto katika utekelezaji wa miradi hiyo huku akisisitiza kazi hiyo ya ujenziwa madarasa kufanyika kwa uwazi, uadilifu, na uwajibikaji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MHE. WASIRA: AJENDA YA SERIKALI NI KUSIMAMIA MAENDELEO YA WANANCHI.

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YAPATA HATI SAFI, MHE. FATMA APONGEZA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA.

    June 13, 2025
  • UFUATILIAJI WAHIMIZWA KWENYE USIMAMIZI WA MIRADI WILAYA YA GEITA

    June 12, 2025
  • MKURUGENZI ASISITIZA HATUA KUCHUKULIWA KUDHIBITI UTORO SHULENI.

    June 05, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa