• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC MAGEMBE "TUWAWEZESHE WANAWAKE KIUCHUMI"

Posted on: March 7th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe ametoa wito kwa jamii, kuwawezesha wanawake katika sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo  ili kuwainua kiuchumi.

DC Magembe ametoa Wito huo kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika Kihalmashauri katika Kata ya Lwamgasa Wilayani Geita Machi 7,  2024.

Katika hotuba yake Magembe amesema kwenye maadhimisho hayo ameshuhudia wanawake waliowezeshwa kiuchumi na kwa sasa wanajitegemea kwa kuendesha kiwanda kidogo.

Amesema hata asasi za mikopo zikiwemo mabenki zinawahimiza wanawake kujiunga Pamoja na kuunda vikundi ambavyo vinaweza kuaminika na kupata mikopo.

Maandamano ya Wananchi mbalimbali waliojitokeza katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliadhimishwa Kihalmashauri katika kata ya Lwamgasa Leo Machi 7, 2024.


Ametumia mhadhara huo, kuwahimiza wanawake kujiunga kwenye vikundi na kwamba mabenki yako tayari kuwakopesha wanawake.

“Tuwawezeshe wanawake kiuchumi, kwenye fursa mbalimbali za kilimo na kadhalika, tumeona pale wakati napita kwenye vikundi mbalimbali tumekuta kuna kikundi cha wanawake, kikundi kile kwasababu kimewezeshwa kimeweza kujenga Uchumi na leo kinajitegemea, leo mpaka wamefikia hatua ya kumiliki kiwanda kidogo” alisema DC Magembe.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe. Khadija Said amemshukuru Mhe. Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyowawezesha wanawake kushika nafasi mbalimbali za uongozi.

Amewataka pia wanawake kutumia vizuri siku ya wanawake Duniani kwa kuhakikisha wanafuatilia mienendo ya Watoto wao ili kujenga Taifa lililo bora.

“Mhe. Mgeni rasmi nichukue nafasi hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, kwa jinsi alivyoweza kutupa nguvu  kinamama wa Tanzania hii kuhakikisha kwamba tunashika nafasi mbalimbali, Lakini kuhakikisha kwamba anatutia ujasiriili tuweze kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi kuhakikisha kwamba tunaboresha familia zetu” alisema Makamu Mwenyekiti Geita DC Khadija.

Wanawake mbalimbali waliojitokeza katika uwanja wa Corona katika kata ya Lwamgasa kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani Leo Machi 7, 2024.


Katika maadhimisho hayo, Pamoja na mambo mengine  Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetoa misaada kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuatambua jitihada za ziada kwenye uelimishaji jamii kuondokana na ukatili wa kijinsia.

Dkt Richard Buchadi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita amesema imefika wakati kauli ya “mwanamke akiwezeshwa anaweza, iachwe na badala yake itambulike kwamba wanawake wanaweza hata bila kuwezeshwa”.

Kwenye Picha wakwanza kulia alieshika kidevu ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Richard Buchad, Katikati ni Mhe. Cornel Magembe Mkuu wa Wilaya ya Geita na WA kwanza kushoto ni Bi. Khadija Said Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Leo Machi 7, 2024 yaliyofanyika Kihalmashauri katika kata ya Lwamgasa.

Dkt. Buchadi Amesema Rais Samia Suluhu Hassana amedhihirisha hilo kwa vitendo kutokana na kazi kubwa alizozifanya hapa nchini.

Aidha kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka huu 2024 ni “Wekeza kwa wanawake, kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii”


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa