• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC KOMBA AWATAKA WAHANDISI KUSIMAMIA VEMA MIRADI YA MAENDELEO-GEITA DC

Posted on: July 30th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba Julai 29, 2024 amefanya Ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika kata ya Kakubilo na Kusikiliza Kero za Wananchi.

Awali akimkaribisha katika kata hiyo Diwani wa kata ya Kakubilo Mhe Kesi Igayo Nyanda ameomba uongozi wa Halmashauri kuwapa kipaumbele mafundi wazawa katika Kutekeleza miradi ya maendeleo katika kata hiyo badala ya kuwa na mafundi wanaotoka nje ya kata hiyo.

Akiwa Katika kata ya Kakubilo Mhe Komba ametembelea Miradi ya Maendeleo katika Kijiji cha Nyabalasana ambapo amekagua ujenzi wa jengo la utawala katika shule ya Sekondari Nyabalasana unaotekelezwa na mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) kwa gharama za Shilingi milioni 100,485,779.88 na kiasi cha shilingi 10,010,000 zikiwa nguvu za wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba amekagua mradi wa jengo la utawala katika shule ya Sekondari Nyabalasana unaotekelezwa na mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) kwa gharama za Shilingi milioni 100,485,779.88 na kiasi cha shilingi 10,010,000 zikiwa nguvu za wananchi.

Kwa upande mwingine Mhe Komba amewataka wahandisi kusimamia vema Miradi ili iwe na kiwango sawa na fedha inayotolewa na Serikali." Kila mtumishi akae kwenye nafasi yake kazi zifanyike vizuri" amesisitiza Mhe Komba.

Mhe Komba akikagua mradi wa zahanati kijiji cha Kabayole kata ya Kakubilo ulionzishwa kwa nguvu za wananchi. Uongozi wa Halmashauri umesema kupitia mapitio ya bajeti, mapato ya ndani na CSR Utawezesha kukamilisha zahanati katika kata hiyo ili kuendelea kusogeza huduma kwa wananchi

Katika kuendelea na Ziara hiyo, Mh Komba ametembelea ujenzi wa Kituo cha Afya Kakubilo ambacho Diwani wa kata hiyo Mhe Kesi Igayo Nyanda ameomba kituo hicho kuanza kutumika ili Wananchi waanze kupata huduma za kiafya ili kupunguza umbali mrefu wa kufuata huduma katika kata za jirani.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba akizungumza na mamia ya wananchi wa Kata ya Kakubilo alipofanya mkutano wa hadhara ambapo amewataka kuacha matendo ya kikatili kwa kukatiza uhai wa watu wenye Ulemavu wa ngozi na kuwataka wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu.

Miradi Mingine ambayo Mhe Komba ametembelea akiwa na wakuu wa Taasisi,Idara na  vitengo ni ujenzi wa zahanati ya kabayole ambao umeanza kwa nguvu za wananchi ambao umesha ezekwa, Zahanati ya Kijiji cha Luhara ambayo ipo hatua ya boma.

Mbali na kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo, Mhe Komba aliweza sikiliza Kero za wananchi na kuzitolea majibu zikiwepo kero za wanufaika wa TASAF ambapo amesema Serikali imetoa maagizo kwa kaya masikini kuwezeshwa pamoja na kuwaletea wananchi Miradi ya Maendeleo katika maeneo yao.

Mradi wa Kituo cha Afya Kakubilo ambao unatarajiwa kuanza kutumika ifikapo Mwezi Septemba 2024. Mradi huo utasaidia kupunguza umbali wa wananchi kufuata huduma maeneo mengine.

Aidha ameitaka Idara ya Maendeleo ya jamii kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya mikopo inayotolewa na Serikali ambayo haina riba ili wananchi waweze kukopa na kuepukana na mikopo almaarufu kama kausha damu.

Akihitimisha ziara katika kata ya Kakubilo Mhe Komba amewasihi Wananchi kuacha matendo ya kikatili kwa kukatiza uhai wa watu wenye Ulemavu wa ngozi na kuwataka wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu. "Kujichukulia sheria mkononi ni jambo ambalo halikubaliki hivyo toeni taarifa kwa Wote wanaojihusisha na tabia za kikatili." amesisitiza Mhe Komba.

Mamia ya wananchi wa kata ya Kakubilo wakifuatilia mkutano wa Hadhara wa Mkuu wa Wilaya ambapo walisikilizwa kero zao na kupatiwa majibu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa