• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC KOMBA ATOA ONYO KALI KWA WATUMISHI WANAOCHEZA NA FEDHA ZA MAENDELEO-GEITA DC

Posted on: May 22nd, 2024

Na: Hendrick Msangi 

WATUMISHI wa umma wasio waadilifu wamepewa onyo kali juu ya matumizi ya Fedha za miradi ya Maendeleo zinazoletwa kwenye maeneo yao.

Akizungumza katika Ziara ya kukagua Miradi ya Maendeleo ndani ya Kata ya Nyarugusu Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe Hashim Abdallah Komba amekemea vikali tabia ya Watumishi wa umma ambao hawatimizi wajibu wao kusimamia Miradi ya Maendeleo.

Aidha ameiagiza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuweka utaratibu wa kukamilisha Miradi iliyo anzishwa kwa nguvu za Wananchi ili kuendelea kuwapa hamasa Wananchi katika Miradi ya Maendeleo.

Katika Ziara hiyo, Mhe Komba ametembelea Miradi ya Maendeleo katika Vijiji vya kata hiyo ambavyo ni Nyarugusu, Ililika, Mawemeru na Kijiji cha Mwabageni ambapo amekagua Miradi ya ujenzi wa zahanati, nyumba za Watumishi na ujenzi wa Shule katika kata hiyo ya Nyarugusu yenye utajiri wa Madini.

Mhe. Hashim Abdallah Komba Mkuu wa Wilaya ya Geita akishirikiana nawananchi wa kata ya Nyarugusu kuchimba msingi kwenye ujenzi wa be Bweni la Wasichana shule ya Sekondari Evarist ambalo lina uwezo wa kubeba wanafunzi 80. Serikali kupitia mfuko wa kunusuru kaya masikini (TASAF) imetoka kiasi cha Shilingi milioni 180 na Wananchi watachangia asiliamia 10 katika ujenzi huo.

Mhe Komba, .amempongeza Diwani wa Kata hiyo Mhe Salehe Juma Msene kwa namna anavyopambana kusukuma Miradi ya Maendeleo katika kata hiyo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro amesema Serikali inatambua juhudi wanazozifanya Wananchi katika ujenzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo na tayari Halmashauri imepeleka orodha ya Miradi ambayo haijakamilika TAMISEMI kwa ajili ya kuratibiwa ili iweze kukamilika na iwanufaishe wananchi.

Pamoja na hayo Ndugu Karia amesema amewaelekeza Wahandisi wa Halmashauri kupita katika kila mradi ili kufanya tathmini ya ukamilishwaji ili kuweza kuwatumia wadau wa Maendeleo katika ukamilishaji wa Miradi hiyo.

Ndg Karia Rajabu Magaro Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita akishirikiana na Wananchi wa kata ya Nyarugusu kuchimba msingi kwenye ujenzi wa Bweni la Wasichana shule ya Sekondari Evarist ambalo lina uwezo wa kubeba wanafunzi 80. Serikali kupitia mfuko wa kunusuru kaya masikini (TASAF) imetoka kiasi cha Shilingi milioni 180 na Wananchi watachangia asiliamia 10 katika ujenzi huo.

Akijibu Kero za Wananchi, Mhe Komba amekemea tabia za rushwa zinazofanywa na Watumishi wa umma baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakilalamikia baadhi ya Watumishi wa Kituo cha Afya Nyarugusu kuomba rushwa kwa wagonjwa wanaoenda kupata matibabu ambapo ameiagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) Wilayani Geita kichunguza tuhuma hizo ili Wananchi hao wapate huduma bora.

Wananchi wa kata ya Nyarugusu wakifuatilia Mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Abdallah Komba alipotembelea kata hiyo kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za Wananchi.

Mkuu huyo wa Wilaya ameendelea kuwasisitiza Watumishi wa umma kushuka chini kusikiliza kero za Wananchi. " Tukishindwa kusimamia kero za Wananchi tutazalisha uvunjifu wa amani" amesema Mhe Komba.

Aidha ameitaka Halmashauri ya Kijiji kutoa taarifa kwa Wananchi juu ya fedha zinazoletwa kwenye maeneo yao kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ili wafahamu na kuendelea kuwa na imani na Serikali yao inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa