• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC KOMBA AITAKA HALMASHAURI KUSIMAMIA WANANCHI KATIKA KUIBUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOKAMILIKA-GEITA DC

Posted on: May 18th, 2024

Na: Hendrick Msangi

NYAMALIMBE MAY 18, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba ameendelea na ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi katika Halmashauri ya wilaya ya Geita May 18 katika kata ya Nyamalimbe inayoongozwa na Mhe Jeremia Ikangaa diwani wa kata hiyo.

Katika ziara hiyo, Mhe Komba ameendelea kuwasisitiza watumishi wa umma kuendelea kusimamia vizuri matumizi ya fedha za serikali zinazopelekwa katika maeneo yao huku akiwataka kushuka chini kuwasikiliza wananchi na kutatua changamoto zinazowakabili kupitia madawati yanayotembea.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Geita  Nicolaus Kasendamila akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndg Karia Rajabu Magaro katika Ziara ya Kukagua Miradi ya Maendeleo kata ya Nyamalimbe.

Pamoja na hayo Mhe Komba amewataka wananachi  kuendelea kudumisha  ulinzi na usalama katika maeneo yao  kwa kuwataka kuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao kwa kutoa taarifa juu ya vitendo vya kiuhalifu na kuwasisitiza kuendelea kujitolea  kwenye shughuli za maendeleo.

Akiwa kata ya Nyamalimbe, Mhe Komba amefanya ukaguzi wa miradi katika kijiji cha  Nyamalimbe, Buzanaki, Lwamizo na Nyamigogo  ambapo amekagua miradi ya afya ikiwepo ujenzi wa jengo la mama na mtoto lililojengwa  kwa nguvu za wananchi kwa kiasi cha Shilingi  9,000,000 na wadau wengine wa maendeleo huku CSR wakiwezesha vifaa vya kuezeka na kulipa mafundi.

Mhe Hashim Abdallah Komba akiwa katika Ziara ya kukagua Miradi ya Maendeleo kata ya Nyamalimbe ambapo amewataka Wananchi kuendelea kijitokeza kuwa mstari wa mbele katika kazi za kujitolea ili kuchochea maendeleo kwani serikali inaendelea kuunga juhudi zao katika kukamilisha miradi ya maendeleo.

Aidha katika kijiji hicho Mh Komba ametembelea nyumba ya mtumishi wa zahanati lilioanzishwa kwa nguvu za wananchi shilingi 8,000,000 na kupata fedha nyingine kutoka kwa Mh Mbunge wa Jimbo la Busanda Mhandisi Tumaini Magesa kiasi cha shilingi 14,000,000.

Miradi mingine aliyoikagua ni pamoja na Ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Lwamizo , ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa zahanati , na kwa upande wa kijiji cha Buzanaki amekagua ujenzi wa jengo la zahanati na nyumba ya mtumishi  zilizo jengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na CSR na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mhe Komba amewataka wananchi kuendelea kijitokeza kuwa mstari wa mbele katika kazi za kujitolea ili kuchochea maendeleo kwani serikali inaendelea kuunga juhudi zao katika kukamilisha miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo ameitaka ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupitia idara ya mipango kuwaongoza wananchi katika kuibua miradi itakayoendana na vipaumbele vya Serikali ili iweze kupata msukumo na kuikamilisha kuliko kuibua miradi mingi isiyokamilika.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Karia Rajabu Magaro amesema Halmashauri itaendelea kushirikiana na Mhe Diwani wa kata hiyo kuipa kipaumbele miradi iliyo anzishwa kwa nguvu za wananchi kulingana na bajeti za Halmashauri.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa