• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC KOMBA AAGIZA MIRADI IANZE KWA WAKATI NA KUKAMILIKA KWA WAKATI -GEITA DC

Posted on: March 19th, 2024

Na: Hendrick Msangi

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba amefanya ziara ya kujitambulisha katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na kuzungumza na watumishi wa Halmashauri.

Mkuu huyo wa Wilaya  amefanya ziara hiyo ikiwa ni mara yake ya kwanza kuzungumza na watumishi wa Halmashauri kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Machi 09, 2024  ambapo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Cornel L.B. Magembe alihamishiwa Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora huku Mhe Hashim Abdallah Komba akihamishiwa Wilaya ya Geita akitokea Wilaya ya Ubungo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu Karia Rajabu Magaro  amesema watumishi hao watazingatia na kufuata maelekezo yote aliyoelekeza Mkuu wa wilaya Mhe Komba

Awali akimkaribisha kuzungumza na watumishi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu Karia Rajabu Magaro alisema Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina jumla ya watumishi 5218 na  kwa upande wa miradi Halmashauri katika kipindi cha miaka mitatu (2021/2022. 2022/2023 na 2023/2024) imetekeleza miradi  yenye jumla ya shilingi 38,932,247,774.25 kutokana na fedha za mapato ya ndani, ruzuku ya serikali kuu pamajo na wa wadau wa maendeleo.

Aidha Karia alisema Halmashauri  kwa mwaka 2023/2024  ililenga kukusanya shilingi 5,135,900,000 na imefanikiwa kukusanya shilingi 6,272,030,392.95 sawa na asilimia 112.25 ambapo kwa mwaka 2023/2024 Halmashauri imelenga kukusanya shilingi 6,774,614,000.00

Akizungumza na watumishi katika Kikao Kazi hicho, Mhe Komba alisisitiza swala la nidhamu na upendo kwa watumishi wa umma ikiwa ni pamoja na kuheshimiana pasipo kujali vyeo na nafasi walizo nazo.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Machi 18, 2024 alipofanya kikao kazi na watumishi hao ambapo aliwataka kutuwa Wabunifu kwa kuwa na mawazo mbadala nje ya majukumu yao ya kila siku. 

Aidha Mhe Komba alieleza mambo ambayo  angependa watumishi hao kuyafahamu ili kuweza  kufanya kazi kwa weledi kuwa ni kuzingatia swala la muda, kuwa wa wazi katika utendaji wao kuepusha migogoro  na kujiepusha na majungu ambayo huondoa ufanisi katika kazi. “Tuwaze kuwa wabunifu  na kuwahudumia wananchi, tunataka watu wafanye kazi” alisema Mhe Komba.

Pamoja na hayo aliitaka timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya kuwa na institutional ownership mechanism, akimaanisha kila mmoja kuimiliki Taasisi ili kuwa na uwelewa mmoja wa shughuli zote za Halmashauri. “Natamani tubebeane mapungufu tusisemeane mapungufu tufanye kazi kwa ushirikiano kuwa na umoja, kupeana taarifa na mrejesho wa kazi ambazo tumepena maana jambo likiharibika linaharibika kwa watu wote” Alisisitiza Mhe Mkuu wa Wilaya.

Akiendelea kuzungumza katika kikao kazi hicho na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mhe Mkuu huyo wa Wilaya alieleza vipaumbele ambavyo angependa watumishi hao wavifahamu ni swala la Mapato na Miradi ya maendeleo ambapo  alisisitiza ukusanyaji wa mapato kwa kila chanzo ili kufikia lengo lililowekwa , kuwa na mfumo wa ukusanyaji wa madeni na kusisitiza kile kinachokusanywa kiache alama kwa kufanya miradi ya maendeleo. “Tuachane na visababu  tuwe watumishi  tunaotaka matokeo, nataka miradi ya maendeleo kuanza  kwa wakati na kukamilika kwa wakati” alisema DC Komba.

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Watumishi hao wametakiwa kutoka kwenye maofisi kwenda kusikiliza kero za wananchi.

Akiendelea kuvitaja vipaumbele vyake, Mhe Komba  aliutaka uongozi wa halmashauri kutatua kero za watumishi na wananchi  kwa kujenga utamaduni wa kuwasikiliza  kwa kuwaheshimu  watu wote wanaofika kupata huduma kwa nafasi zao pasipo kuwadharau na kuwataka kutoka kwenye ofisi kwenda kusikiliza kero za wananchi.

Pamoja na vipaumbele hivyo, alisisitiza swala la ulinzi na usalama akiwataka watumishi hao kutokuzipuuza hisia za wananchi pale wanapukuwa na manung’uniko na kuwataka kutoa taarifa zote zinazopelekea viashiria vya uvunjifu wa amani,

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba akiwa ndani ya ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndugu Karia Rajabu Magaro alipotembelea Halmashauri ya Wilaya Machi 18.2024 ambapo alizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Mwisho Mkuu wa Wilaya aliwataka watumishi kuwa  wabunifu  kwa kuwa na mawazo mbadala nje ya majukumu yao ya kila siku ili kuweka alama (Extra ordinary Perfomance) kwenye utendaji kazi wao wa kila siku.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa