• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

CHANJO KWA WATOTO KUPEWA KIPAUMBELE

Posted on: February 6th, 2025

Wahudumu wa Afya na Lishe Wilayani Geita, wamehimizwa kutoa elimu sahihi juu ya umuhimu wa chanjo kwa watoto, ili kuondokana na tatizo la magonjwa nyemelezi pindi mtoto akiwa katika hatua za ukuaji.

Akizungumza hapo jana kwenye Kikao cha tathmini ya taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe Octoba-Disemba 2024, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Geita, Katibu Tawala Bi Lucy Beda amesema kuwa ni muhimu kwa akina mama kupewa elimu ya kutosha juu ya Utoaji wa Chanjo kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano.

"Lazima akina mama wapewe elimu juu ya umuhimu wa kuwapa watoto chanjo. Hii itasaidia kupunguza vifo miongoni mwa wawoto pamoja na kuwa na usatwi kwenye jamii yetu." Amesema Bi. Lucy Beda.

Katibu Tawala Bi Lucy Beda akihudhuria zoezi la upimaji wa presha kwa hiari lililoratibiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Geita, kabla ya kuanza kwa Kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Lishe, Octoba-Disemba katika ukumbi wa EPZ, Bombambili.

Aidha, Bi. Beda aligusia pia kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Marbug nchini, ambapo ameagiza elimu iendelee kwa usahihi maeneo ya magereza, mashuleni, pamoja na maeneo yenye mikusanyiko ya watu kama Katoro na Nkome, huku akizitaka Halmashauri ziratibu vikao vya afya kwa wakati.

Kwa upande mwingine, Afisa Lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya, Geita, Bi. Nasim Ginga amesema kuwa, katika kipindi cha robo ya pili, Oktoba-Disemba, jumla ya watoto 14,361 Kati ya 15,381 chini ya mwaka mmoja, sawa na 93%, wameweza kupatiwa chanjo.

Afisa Lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Bi Nasim Ginga amesema kuwa kwa mwaka 2024, Halmashauri ilifanikiwa kutoa chanjo kwa watoto 59,735 kati ya 61,528 chini ya mwaka mmoja, sawa na  97%.

Miongoni mwa mikakati ambayo ipo kwaajili ya kuinua kiwango cha utoaji wa chanjo kwa kipindi cha Januari-Machi 2025, ni pamoja na kuendelea kushirikiana na viongozi ngazi ya vijiji na mitaa kutoa elimu juu ya umuhimu wa chanjo kwa jamii, huku pia kukiwa na lengo la kuimarisha utoaji wa chanjo kwa njia ya huduma za mkoba katika maeneo magumu kufikika kama visiwa na machimbo madogo kupitia Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi, na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM).

Baadhi ya Wajumbe wa Kikao  cha Tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Lishe, wakifuatilia mada mbalimbali.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa