• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAPITISHA RASIMU YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2022/2023 YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 81

Posted on: January 25th, 2022

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Januari 25, 2022 limejadili na kupitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 inayopendekeza kukusanya na kutumia jumla ya shilingi bilioni 81, milioni 151,laki 7, 22 elfu na 890. (Tshs.81,151,722,890)

Akiwasilisha Rasimu hiyo ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita John Paul Wanga amesema katika jumla kuu  ya Tshs. 81,151,722,890 kiasi cha Tshs. 12,836,814,969 ni fedha za ruzuku zitakazotumika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo na Tshs. 3,003,960,860 ni ruzuku zitakazotumika kwa matumizi ya kawaida.

Rasimu hiyo imeendelea kufafanua kuwa kiasi cha Tshs.55,183.993,000 zitatumika kulipa mishahara ya  watumishi huku kiasi cha Tshs 4,486,875,000 ni makusanyo ya ndani ukiondoa mapato fungani.

Aidha Rasimu hiyo imebainisha kuwa kiasi cha Tshs. 2,692,125,600 ni matumizi ya kawaida ya mapato ya ndani na kiasi cha Tshs.1,794,750,400 ni mapato ya ndani kwa ajili ya shughuli za maendeleo huku kiasi cha Tshs. 510,844,000 ikiwa ni mapato mengine ambayo ni kama vile CHF, NHIF, DRF, Tozo za minara mashuleni na ada kwa kidato cha tano na sita.

Miongoni mwa vipaumbele vilivyozingatiwa katika Rasimu hiyo ni pamoja na kuboresha huduma za jamii kupitia sekta za Elimu, Afya, Ardhi, Mifugo na Uvuvi, Kilimo, na Maendeleo ya Jamii.

Wakati huo huo Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika kuandaa na kutekeleza mpango na bajeti ya mwaka 2022/2023 imepanga kushirikiana na wadau mbalimbali kama vile GGML, BUCKREEF, NELICO, PLAN INTERNATIONAL, MDH, KIVULINI, SONGAMBELE, ICAP, CODERT, na SEDIT.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu ameshauri idara ya maendeleo ya jamii kutoa mikopo mikubwa kwa watu wachache ili iwe na tija zaidi,  kuliko kugawanya kidogo kidogo kwa watu wengi suala linalochelewesha matokeo chanya huku akiwataka kutoa elimu kwa vikundi vyenye mikopo hiyo kurejesha kwa wakati ili na makundi mengine yanufaike.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa