• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI LAAZIMIA KUKAMILISHA MIRADI VIPORO KUPITIA CSR NA MAPATO YA NDANI

Posted on: February 15th, 2024

Na Hendrick Msangi

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Februari 13 na 14 katika kikao chake cha kawaida limepokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Serikali ngazi ya Kata na uwasilishaji wa taarifa za kamati ya fedha uongozi na mipango, kamati ya uchumi,ujenzi na mazingira, kamati ya elimu afya na maji pamoja na kamati ya kudhibiti Ukimwi kwa kipindi cha Octoba hadi Disemba 2023.

Jumla ya Kata 37 ziliwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za serikali katika maeneo yao ambapo Madiwani hao walijika kwenye changamoto mbalimbali zikiwemo za  upungufu wa watumishi katika sekta ya elimu na afya, kuharibika kwa miundombinu ya barabara pamoja na ucheleweshwaji wa vifaa kwa ajili ya kukamilisha miradi inayotekelezwa na CSR kunakopelekea mafundi kukaa site mda mrefu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu akiwa na Makamu  mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe Hadija Said Joseph wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri.

Awali akifungua kikao hicho, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu aliwataka madiwani hao kuzingatia kanuni za uendeshaji wa kikao hicho ili kufikia lengo la kikao hicho.

Akizungumza katika Baraza hilo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu Karia Rajabu Magaro aliwasihi Madiwani hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili kuendelea kufuata taratibu zote na kuzizingatia kwa manufaa ya Halmashauri. “Mahali popote mnapo ona kuna uvujaji wa Mapato tufahamishane ili kuchukua hatua za ufuatiliaji kwa manufaa ya Halmashauri” alisema Magaro.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu Karia Rajabu Magaro akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani ambapo amewasihi waheshimiwa madiwani kuendelea kutoa ushirikiano ili Halmashauri hiyo iendelee kukusanya mapato katika vyanzo vyake

Aidha aliwasihi Madiwani hao kuendelea kutoa ushirikiano kufuatilia wazazi ambao hawajawapeleka watoto shule ili kuendelea kuinua kiwango cha ufaulu huku akitaja kiwango cha ufaulu kwa mitahani ya Kitaifa kwa kidato cha pili na cha nne kwa mwaka 2023 kuongezeka ambapo kwa kidato cha pili kiwango cha ufaulu kikiwa ni asilimia 83.47 kulinganisha na mwaka 2022 ambapo kiwango cha ufaulu kilikuwa asilimia 82.7 sawa na ongezeko la asilimia 0.77

Na kwa upande wa kidato cha nne kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 9.14 ambapo mwaka 2022 ufaulu ulikuwa asilimia 77.80 kulinganisha na matokeo ya mwaka 2023 ambapo ufaulu umekuwa asilimia 86.81

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita ndugu Cornel L.B Magembe alizitaka Taasisi za RUWASA, TARURA na TANESCO kuhudhuria kwenye vikao vya kamati za Madiwani na Watumishi wa Halmashauri ili kuweza kuwa na taarifa zenye utoshelevu kuwafikia wananchi,

Akizungumzia swala la miradi viporo, Magembe  alisema ni vema ikamilishwe kwa ajili ya kuwapelekea wananchi huduma “Tuweke nguvu ya ziada kukamilisha miradi ambayo ni viporo na kuacha kuanzisha miradi mipya ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya utekelezaji  wa miradi ya CSR iliyopita” alisema  Magembe.

Kuhusu upungufu wa walimu wa kike, Magembe alisema ipo haja ya kuhamisha walimu hao kwa shule ambazo wapo wengi na kuwapeleka kwenye shule zenye upungufu hivyo kuitaka halmashauri kuweka bajeti kwenye mapato yake ya ndani kwa ajili ya zoezi hilo ambapo ofisi ya Mkurugenzi ilisema itaendelea kuweka msawazo wa walimu wa kike ambapo jumla ya shule za msingi 18 hazina walimu wa kike na 14 za sekondari

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Komredi Barnabas Mapande alilitaka baraza hilo kuhakikisha miradi viporo inakamilishwa kwa wakati ili kuwaondolea wananchi kero na kuepuka kuanzisha miradi mipya kwani wananchi wanahitaji miradi iliyokamilika ili kuendelea kuwa na Imani na serikali yao.”Tutumie fedha za CSR kukamilisha miradi yetu” alisema Mapande

Kufuatia upungufu wa walimu wa Kike Mapande alisema ipo haja ya mkoa wa Geita kuiomba Serikali kuongeza walimu wa kike kwani upungufu wa walimu hao unasabisha watoto wa kike kukosa msaada pale inapobidi.

Kuhusu swala la miundombinu ya barabara kuwa mibovu  na kutokukamilika kwa wakati,Meneja wa  TARURA  Mhandisi Bahati Subeya alisema  pamoja na changamoto ambazo zinajitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi zikiwepo mvua zinazoendelea kunyesha, baadhi ya wananchi kuziba mifereji ya kutolea maji ya mvua pamoja na ufinyu wa bajeti ukilinganisha na mahitaji halisi ya matengenezo ya barabara ofisi ya TARURA itaweka kwenye mpango wa  bajeti zijazo kulingana na ukomo wake kwa ajili ya utekelezaji kwa kuwa miundombinu mizuri ya barabara huinua uchumi wa halmashauri.

Kwa upande wa huduma za Maji safi na salama, Ofisi ya RUWASA ilisema ni vema Madiwani hao kuendelea kuzisimamia shule, Zahanati na vituo vya afya kulipa gharama za maji ili kuisaidia RUWASA kuendelea kuendesha miradi ikiwa ni pamoja kusaidia kulinda vifaa vinavyopelekwa kwenye miradi kwani kumekuwa na tabia ya wizi wa vifaa hivyo ili kuendelea kunuifaika na maji safi na salama.

Kuhusu Mradi wa Kimkakati wa Soko la Katoro, Madiwani hao waliazimia kupunguza bei ya pango kwenye soko hilo ili kuendelea kuvutia wananchi kwa ajili ya kufanya biashara katika soko hilo huku wakishauri Masoko ya dhahabu kuhamishiwa kwenye soko hilo ikiwa ni pamoja na kutengeneza miundombinu ya barabara inayoelekea kwenye soko hilo ili magari yaweze kufika eneo hilo ambapo Halmashauri itaongeza mapato.

Waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakifuatilia kikao cha robo ya pili ambapo kwa pamoja waliazimia kushusha bei za pango kwa soko la kimkakati la Katoro ili kuendelea kuwavutia wafanya biashara kuwekeza katika soko hilo

Akihitimisha kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu aliwataka watendaji wa Halmashauri kuendelea kuweka bidii kwenye ukusanyaji wa mapato ili kutumia fedha za mapato ya ndani kuendelea kukamilisha miradi viporo. “Sitavumilia kuona mapato yanashuka, kwani fedha hizo ndio ndio zitatusaidia kutatua changamoto za wananchi” alisema Kazungu.

Aidha Mhe Kazungu aliwataka Waheshimiwa madiwani kushirikiana na wazazi kuhakikisha watoto ambao hawajaripoti kidato cha kwanza licha ya kufaulu waweze kuripoti haraka iwezekanavyo kwani gharama za elimu zipunguzwa na Serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku akisisitiza swala la lishe kuwa ni la lazima na sio la hiyari na kuwataka madiwani hao kuendelea kuhamasisha wazazi ili watoto wasipatwe na udumavu ambao unaweza kuepukika.

Kufuatia kikao chake hicho cha kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za Serikali kwa kipindi cha Octoba hadi Disemba, Baraza la Madiwani limewafukuza kazi watumishi watatu kwa sababu za utoro kazini, huku watumishi wawili wakipewa onyo kali na mtumishi mmoja kutakiwa kufanya kazi yalipo makao makuu ya Halmashauri hiyo kwa kuendelea kuangaliwa mwenendo wake wa utekelezaji wa kazi.

Madiwani hao wameiomba Serikali sikivu ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kuendelea kuziunga mkono nguvu za Wananchi katika ujenzi wa Miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili kusaidia kuinua ari ya wananchi ya kujitolea katika shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye maeneo yao.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa