• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA LAPONGEZWA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: August 7th, 2024

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Agosti 7, 2024 limeendelea na kikao chake cha kawaida kwa siku ya pili ambapo kamati za Baraza hilo zimewasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za serikali kwa robo ya nne April hadi Juni 2024.

Kamati zilizowasilisha taarifa ni pamoja na Kamati ya Fedha, uongozi na Mipango, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Elimu, Afya na Maji, Kamati ya Kudhibiti UKIMWI na Kamati ya Maadili.

"Tusimamie mashine za kukusanya mapato ya serikali (Posi) kwa kuzingatia matumizi ya posi na tujiwekee mikakati mapema ili makusanyo yetu yaweze kwenda vizuri"Hashim Abdallah Komba Mkuu wa Wilaya ya Geita

Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye pia ni diwani wa kata ya Butobela Mhe. Charles Kazungu amewapongeza madiwani wa Kata zote 37 kwa ukusanyaji mzuri wa mapato Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 uliopelekea Halmashauri kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 7.3 sawa na asilimia 107.88

Tuendelee kusimamia kukusanya mapato yetu kwa haki kwa kufuata sheria , kanuni na taratibu bila kumuumiza mfanyabiashara na mwananchi yeyote .Ndg Karia Magaro Mkurugenzi Mtendaji

Aidha Mhe. Kazungu amewasisitiza madiwani wote kufanya kazi kwa bidii zaidi kwa mwaka mpya wa fedha 2024/2025 ili kuweza kukusanya mapato ya kutosha katika maeneo yao. "Niwaombe sana kasi ile tuliyokuwa nayo 2023/2024 tuende nayo 2024/2025 tena kwa kasi ya 5G". Amesisitiza Mhe. Kazungu katika kikao cha baraza hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Abdallah Komba amewasisitiza madiwani wa Kata zote kushirikiana vema na vyombo vya usalama  ili kuweza kulinda hali ya ulinzi na usalama katika maeneo yao kutokana na kuwepo kwa matukio mengi ya kihalifu kama vile uporaji, ukabaji, pamoja na vitendo vya kikatili  kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.

"Nawapongeza kwa ukusanyaji wa mapato na miradi inayoendelea kufanyika. Pia Mkurugenzi kwa namna ambavyo unawaunganisha watumishi kukaa pamoja na kuendelea kutenda haki kunakopelekeawatumishi kufanya kazi na chama cha mapinduzi (CCM) kitaendelea kuwa pamoja na serikali" Komredi Barnabas Mapande Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Geita

Sambamba na hayo Mhe. Komba amelipongeza baraza la madiwani kwa kazi nzuri wanayoifanya ikiwa ni pamoja na ukusanyaji mkubwa wa mapato yanayowawezesha kuendesha shughuli mbalimbali za kimaendeleo na ushirikiano walio nao katika kuisaidia Halmashauri kufikia malengo yake.

Naye Mbunge wa Jimbo la Busanda Mhandisi Magesa ameiomba kamati ya ulinzi na usalama kuendelea kuimarisha  ulinzi na usalama katika Kata ya Butundwe kwa kushughulikia kikamilifu suala la wizi na kuuliwa kwa ngo'mbe pamoja na viboko ambao wamekua tishio katika ukanda huo kutokana na kusababisha vifo kwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo."Niiombe kamati ya ulinzi na usalama iwasaidie Wananchi wa kata ya  Butundwe kupambana na viboko hao kwani wamekua tishio kutokana na matukio mengi yanayoendelea kutokea kila leo". Amesema Mhe. Magesa

"Niwaombe kasi ile ile ya  mwaka 2023/2024 tuendelee nayo kwa kasi zaidi kwa mwaka 2024/2025 tujifunge mkanda ili tuendelee kukusanya zaidi." Mhe Charles Kazungu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Vilevile Baraza la madiwani katika kikao hicho limeazimia kuwarejesha kazini Ndg Mick Chotta aliyekuwa mtumishi kitengo cha sheria pamoja na Ndg Abdallah Mkumbo aliyekuwa Afisa utumishi daraja la kwanza ambao walisimamishwa kazi Kutokana na mashauri ya kinidhamu. Hatua hiyo imefikiwa kutokana na uchunguzi uliofanyika kupitia kamati mbalimbali ikiwemo kamati za madiwani na kubaini kukosekana kwa hatia kwa watumishi hao.

Katika baraza hilo, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Magaro amewaomba Waheshimiwa madiwani kuendelea kushirikiana  katika kusimamia miradi ya maendeleo inayoendelea katika maeneo yao  kwa ufanisi na ubora uliokusudiwa  na kuwahikikishia kuendelea kuwa bega kwa bega na timu ya menejimenti ya halmashauri

Aidha Ndg Magaro ameendelea kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania kwa  kuendelea kuleta fedha nyingi za miradi  ambayo imepunguza adha kwa wananchi na kuwataka madiwani  kuendelea kujitoa ili malengo ya Halmashauri yaendelee kutimia kwa mwaka 2024/2025.

kikao cha baraza la madiwani Agosti 7 kujadili taarifa za maendeleo ambapo jumla ya kamati 5 ziliwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Baraza hilo limehudhuriwa na viongozi mbali mbali wa chama na serikali akiwepo kamati ya Ulinzi na Usalama ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba, Katibu tawala wilaya Bi Lucy Beda, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Cde Barnabas Mapande, Waheshimiwa wabunge wa Jimbo la Geita vijijini Mhe Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Jimbo la Busanda Mandisi Tumaini Magesa, wakuu wa Idara na Vitengo, kikundi cha vijana wajasiriamali Halmashauri ya Geita na wakuu wa taasisi za umma,

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa