• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA LAFUNGA HESABU ZAKE KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

Posted on: August 30th, 2024

Na: Nyamizi Elias

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita likiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Charles Kazungu Agosti 29, 2024 limefanya kikao chake maalum cha uwasilishaji wa hesabu za mwisho kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Akiwasilisha taarifa ya ukamilishwaji wa hesabu hizo Mweka hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Eveline Richard amesema, kazi ya uwasilishwaji wa hesabu ya mwaka 2023/2024 ilianza mapema Julai 2024 na kukamilika rasmi Agosti 25, 2024.

Waheshimiwa Madiwani wakiwa  katika Kikao cha Baraza Maalum la ufungaji wa hesabu  za Sererikali kwa upande wa Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Aidha Bi Eveline ameeleza kuwa hesabu za fedha kwa mwaka wa fedha 2023/2024 zimegawanyika katika maeneo tofauti tofauti ambayo ni taarifa mbalimbali za Halmashauri, maelezo ya jumla ya fedha kwa mwaka wa fedha 2023/2024 pamoja na taarifa za hesabu kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Eveline Richard akiwasilisha taarifa ya ufungaji wa hesabu kwa  mwaka wa fedha 2023/2024.

Vilevile Bi Eveline  katika uwasilishaji wake amechanganua zaidi mgawanyiko wa fedha kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa kuonesha fedha zilizokuwepo kuishia Juni 30, 2024 ni kiasi cha shilingi Bilioni 9.5, wadaiwa wa Halmashauri shilingi Bilioni 8.17, Uwekezaji mfuko wa Serikali za mitaa ni shilingi 87.3, Mali za  Halmashauri zisizohamishika ni shilingi Bilioni 90.49, wadaiwa wa Halmashauri ni shilingi Bilioni 1.76 pamoja na kuonesha mapato na matumizi ya Halmashauri ambapo mapato ni jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 85.8 huku  matumizi ikiwa ni shilingi Bilioni 87.5.

Katibu Tawala  wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita  Bi Lucy Beda akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Magaro wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani la uwasilishaji wa taarifa ya Ufungaji wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo Mkurugenzi Mtendaji  amelipongeza baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa ukusanyaji mzuri wa mapato uliochochea kukamilisha kwa wakati uandaaji wa taarifa ya hesabu ya mwaka wa fedha 2023/2024.

Mbali na hayo Bi Eveline pia ameeleza dhima na madhumuni ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ikiwa ni pamoja na kuendeleza ubora wa elimu ya Msingi na Sekondari, ubora wa huduma za afya, kubaini vyanzo vipya vya mapato pamoja na kuboresha ukusanyaji na usimamizi wa matumizi.

Katika kuwasilisha taarifa hiyo, Mweka hazina huyo amewashukuru viongozi na wadau wote wa ukusanyaji wa mapato kwa ushirikiano waliouonesha katika kuhakikisha wanakamilisha uwasilishwaji wa taarifa ya hesabu ya mwaka wa fedha 2023/2024.

Kwa upande wake Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Geita Komredi Gabriel Masunga ameupongeza uongozi mzima wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa uchapakazi bora katika ukusanyaji wa mapato na kuwaasa wananchi kuendelea kuwapa ushirikiano viongozi wao ili kuweza kukusanya mapato zaidi kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Akizungumza Katika Baraza hilo Katibu tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda amelipongeza Baraza la Madiwani, Mkurugenzi Mtendaji na watendaji  kwa uchapaji kazi mzuri wenye ufanisi unaongeza mapato katika Halmashauri.

Waheshimiwa Madiwani wakiwa  katika Kikao cha Baraza Maalum la ufungaji wa hesabu  za Sererikali kwa upande wa Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Pamoja na hayo , Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Magaro ameishukuru Serikakali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt  Samia Suluh Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo kwa kutoa fedha kwa watumishi pamoja na kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akihitimisha kikao hicho Mwenyekiti wa baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu amewasihi Waheshimiwa  Madiwani kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wakusanyaji wa mapato ili kuweza kutimiza malengo waliyojiwekea ya kukusanya mapato zaidi kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa